• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtanda awakaribisha wananchi mapokezi ya Mwenge

Posted on: July 3rd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amewakaribisha viongozi, watendaji na wananchi wote wa Mkoa wa Mara kushiriki katika mapokezi, mbio na mkesha wa Mwenge wa Uhuru wakati wote utakapokuwa katika Mkoa wa Mara.

Mkuu wa Mkoa amesema hayo leo tarehe 3 Julai, 2023 wakati alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Mara yatakayofanyika kesho katika viwanja vya Shule ya Msingi Robanda, Wilaya ya Serengeti.

“Ninawaomba viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru lakini pia katika mbio zake na mikesha itakayofanyika katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuanzia kesho hadi tarehe 12 Julai, 2023”amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa Mkoa wa Mara umejiandaa vizuri kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliojitolea kwa hali na mali.

Mhe. Mtanda amewahakikishia wananchi kuwa katika mapokezi, mbio na mikesha na sehemu zote mwenge utakakopita kutakuwepo na burudani na usalama wa kutosha ili kuwawezesha wananchi kuushangilia Mwenge wa Uhuru kwa amani.

Awali, akizungumza katika kikao cha maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru Mhe. Mtanda amewataka viongozi, wadau na watumishi wote walioalikwa kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru bila kukasa.

Aidha, Mheshimiwa Mtanda ameitaka Kamati ya Maandalizi ya Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Mara kutekeleza majukumu yake kama ilivyopanga na kuhakikisha mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yanafana na kuwa mfano wa kuigwa.

Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa katika Mkoa wa Mara kesho ukitokea Mkoa wa Arusha ambapo utakimbizwa hadi tarehe 12 Julai, 2023 na tarehe 13 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa kwa Mkoa wa Mwanza katika eneo la Nansio, Ukerewe.

 Kesho Mwenge wa Uhuru baada ya kupokelewa anza mbio zake kwa kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na mkesha wa Mwenge wa Uhuru utakauwa katika mji wa Mugumu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.