• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi azindua zoezi la ugawaji wa fidia Nyatwali

Posted on: September 6th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo tarehe 5 Septemba, 2024 amezingua zoezi la utoaji wa fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda wanaohama kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Mtambi amesema Serikali imeruhusu wananchi hao kupata nyongeza ya fidia yao kwa asilimia 7 baada ya malipo hayo kuchelewa baada ya tathmini ya eneo hilo kukamilika kutokana na sababu mbalimbali na kuwahamasisha kuondoka mapema baada ya kupata malipo yao.

“Ni vizuri mkipata pesa ya fidia kabla hamjaanza kufanya mambo mengine muondoke mapema katika eneo hili kabla ya fedha mnazopata hamjatumia kwenye mambo mengine yasiyo na msingi” amesema Mhe. Mtambi.

Amewataka viongozi wa eneo hilo kuonyesha mfano kwa kuanza kuondoka mapema na kuzitaka familia kujadili kwa undani namna ya kwenda kujenga familia zao katika maeneo mengine watakayoamua kwenda kuanzisha maisha yao.

Mhe. Mtambi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele cha malipo ya fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali na kuwawezesha wananchi hao kwenda kuishi maisha yao katika mazingira salama mbali na wanyama wanaotoka katika hifadhi.

“Hili ni eneo la mapito ya asili ya wanyama na ambalo lina manufaa makubwa katika ikolojia na fursa mbalimbali za utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Ziwa Victoria” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Robert Maboto ameipongeza Serikali kwa kukamilisha mchakato wa malipo na kuiomba Serikali kutoa elimu ya kutosha ya namna zoezi la ulipaji wa fidia litakavyofanyika.

“Wananchi hawa wapo tayari kusikiliza maelekezo ya Serikali kuhusiana na zoezi hili tuwaeleweshe vizuri wananchi ili kuondoa malalamiko ya wananchi hapo baadaye” Mhe. Maboto.

Kwa upande wake, mwananchi wa Mtaa wa Kariakoo katika Kata ya Nyatwali amesema Bibi Mgesi Kisuka Machira ameishukuru Serikali kwa kutoa malipo hayo waliyokuwa wanayasubiri kwa muda mrefu na kuahidi atahama eneo hilo mapema iwezekanavyo.

“Tunamshukuru Rais kwa kutoa malipo ya kuhamishwa, kero za wanyama waharibifu tutaondokana nazo ikiwemo kuvamiwa na mamba, kiboko, tembo na wanyama wengine mara kwa mara” amesema Machira.

Bibi Machira ambaye ndiye amekabidhiwa Washima amesema amefurahia kwa kuwa Serikali imewaruhusu kwenda na vitu vyote walivyokuwa navyo ikiwemo matofali, mabati na miti ambavyo watavitumia huko wanakoenda.

Zaidi ya wananchi 3,500 wa Kata ya Nyatwali wanategemea kulipwa fidia na Seriklai kupitia Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ambapo jumla ya shilingi 45.9 kimetengwa kwa ajili ya malipo ya wananchi kutokana na eneo hilo kupitiwa na wanyamapori kutoka SENAPA wakati wa kiangazi wanapokwenda kunywa maji Ziwa Victoria katika ghuba ya Speke.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.