• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi awataka wananchi kuchangamkia fursa ya Madaktari Bingwa

Posted on: November 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepokea awamu ya pili ya Madaktari Bingwa 63 wa Mama Samia na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa za uwepo wa Madaktari Bingwa kupata huduma za kibingwa katika maeneo yao.

Akizungumza katika mapokezi hayo, Mhe. Mtambi amesema Serikali imewasaidia wananchi na badala ya wagonjwa kwenda kwenye hospitali za rufaa ambazo zipo mbali kupata huduma za kibingwa, wanapata huduma za kibingwa na kibobezi katika maeneo yao baada ya Serikali kufanya maboresho makubwa katika sekta ya afya.  

“Hii imewezekana kwa sababu Serikali imeboresha miundombinu na vifaa tiba na watumishi katika Hospitali za Halmashauri na vituo vya afya na kuwezesha madaktari bingwa kuweza kutoa huduma katika Hospitali hizo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema madaktari hawa watatoa huduma katika Hospitali ya Manispaa ya Musoma, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime, Hospitali ya Nyamwaga, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Hospitali ya Wilaya ya Rorya.

Aidha, madakatari hao watatoa pia huduma katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Hospitali ya Manyamanyama (Bunda Mjini), Kituo cha Afya Ikizu na Kituo cha Afya Kasahunga vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Kwa mujibu wa Mhe. Mtambi magonjwa yatakayotibiwa na madaktari hawa ni magonjwa ya wanawake na uzazi, watoto na watoto wachanga, magonjwa ya ndani kama vile kisukari, presha na kadhalika, upasuaji na matatizo ya mfumo wa mkojo na magonjwa ya kinywa na meno.

Mhe. Mtambi ametoa rai kwa wataalamu wa afya wa Mkoa wa Mara kusimamia na kuratibu vizuri zoezi hili ili wananchi wenye changamoto waweze kupata huduma stahiki na kwa wakati na kwa kuzingatia maelekezo na miongozo ya Serikali.  

Mhe. Mtambi amewakaribisha sana madaktari bingwa katika Mkoa wa Mara na kuwataka kabla ya kuondoka watembelea kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kula nyama choma na kichuri katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Afya Dkt. Joakim Masunga ameeleza kuwa Halmashauri zote zimepangiwa Madaktari Bingwa na Wauguzi Bingwa watakaosaidia kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi kulingana na mahitaji.

Dkt. Masunga ameeleza kuwa madaktari hao wanatarajiwa kuanza kutoa huduma kuanzia leo hadi tarehe 16 Novemba, 2024 na wanategemewa kutumia muda wao kushughulikia matatizo mbalimbali ya wagonjwa.

Dkt. Masunga amesema madaktari hao bingwa wakiwa katika Hospitali hizo watawajengea uwezo watumishi wa sekta ya afya katika maeneo mbalimbali, watasaidia kupunguza rufaa za wagonjwa na kuongeza mapato ya hospitali hizo.

Dkt. Masunga ameeleza kuwa madaktari hao watatoa huduma katika vituo hivyo kuanzia tarehe 11 Novemba, 2024 hadi tarehe 16 Novemba, 2024 na watafanya kazi katika muda wa kawaida wa kazi wa hospitali za Halmashauri na vituo vya afya.

 Hafla mapokezi ya madaktari hayo imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Menejimenti ya Sektretarieti ya Mkoa wa Mara, Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, Wakurugenzi wa Halmashauri, Timu ya Usimamizi wa Sekta ya Afya Mkoa wa Mara (RHMT) na Waganga Wakuu wa Halmashauri.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.