• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi awataka wanamara kuishangilia Biashara United kesho

Posted on: June 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ametembelea kambi ya mazoezi ya Timu ya Biashara United na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu hiyo itakapokuwa inacheza na timu ya Tabora United tarehe 12 Juni, 2024 katika Uwanja wa Karume, Manispaa ya Musoma.

“Baada ya kuangalia mazoezi yao ninaamini kesho watafanya vizuri, wageni wategemee bakuri la kichuri…..Ninawaomba wananchi tujitokeze kwa wingi kuishangilia timu yetu uwanjani wakati inatoa dozi za kichuri kwa wapinzani wao” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameipongeza timu hiyo kwa maandalizi mazuri ya mchezo huo na kuwataka wachezaji kucheza vizuri na kuifunga timu ya Tabora United na kuwaahidi kuwa atakuwepo uwanjani kuangalia michuano hiyo.

Amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu hiyo ili iingie kwenye michuano ya ligi kuu na kuweza kuzileta timu kubwa kucheza katika Uwanja wa Karume jambo ambalo litaibua fursa mbalimbali za kijamii na kibiashara katika Mkoa wa Mara.

“Nikiwaangalia hawa wachezaji ninauona ushindi mkubwa kesho, wananchi mje uwanjani muone timu yetu ikitoa kichuri kwa Tabora United na timu zote zitakazokuja kucheza michezo yake katika Uwanja wa Karume” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Kocha ya Timu ya Biashara United Bwana Amani Josia amemshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa kuja kuitembelea kambi yao na kuwatia moyo wachezaji wa timu hiyo kabla ya mechi hiyo muhimu kwa timu yao.

Bwana Josia amesema wanategemea upinzani kuwa mkubwa kwa sababu timu pinzani inatoka ligi daraja la kwanza na kwa kupoteza mechi hiyo itakuwa haiwezi kucheza tena ligi kuu katika msimu ujao wa ligi.

Bwana Josia amesema wachezaji wa Biashara United wanajitoa kuhakikisha ushindi unapatikana katika mechi hiyo na mechi ya marudio ambayo inatarajiwa kuchezwa hivi karibuni.   

Mechi ya Biashara United na Tabora United mechi ya mchujo (play offs) katika Ligi Kuu ya NBC ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kuamua timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania kwa msimu ujao na mchezo wa marudio baina ya timu hizi mbili unatarajiwa kufanyika tarehe 19 Juni, 2024.

 Timu ya Biashara United inapambana kuwania kucheza ligi kuu baada ya kupita kwenye mchujo wa ligi ya Championship na kuwa miungoni mwa washindi wa ligi hiyo kutokana na kuwa na wachezaji ambao wameshawahi kucheza kwenye ligi kuu katika misimu iliyopita.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.