• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi awataka wadau kuhamasisha amani

Posted on: October 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha wadau wa uchaguzi kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 katika ukumbi wa Uwekezaji na kuwataka wadau wa uchaguzi kuhakikisha kuwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanyika kwa amani na utulivu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amewataka wadau wote kushiriki kikamilifu katika kuwahamasisha wananchi kushiriki katika matukio muhimu ya uchaguzi kwa amani na kufuata miongozo inayotolewa na wasimamizi wa uchaguzi.

“Katika uchaguzi huu tunahitaji amani na utulivu, vyama na wagombea wanadi sera zao na kuwashawishi wananchi wawachague na Serikali ya Mkoa tutahakikisha tunaweka mazingira mazuri ya uchaguzi” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024 na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili wapate haki ya kupiga na kupigiwa kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa maana wasipojiandikisha hawataweza kupiga kura.

Kanali Mtambi amesema sifa za mtu anayepaswa kujiandikisha ni; awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, mkazi wa Mtaa, Kijiji au Kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika na kuongeza kuwa orodha ya wapiga kura itabandikwa kwenye mbao za matangazo na Msimamizi wa Uchaguzi tarehe 21 Oktoba, 2024 ambapo watakaoonekana kwenye orodha hiyo ndio watakaoruhusiwa kupiga kura.

Mhe. Mtambi amesema zoezi la kuchukua na kurejesha fmu za kugombea nafasi za uongozi litafanyika tarehe 01-07 Novemba, 2024 na kuzitaja nafasi zonazogombewa kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa, Wajumbe wa Kamati ya Mtaa (kundi mchanganyiko) na kundi la wananwake kwa Halmashauri za Miji na Manispaa.

Kwa Halmashauri za Wilaya, nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti wa Kijiji, Wenyeviti wa Vitongoji vilivyomo katika eneo la kijiji, wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji (kundi mchanganyiko) na kundi la wanawake.  

Mhe. Mtambi amesema zoezi la uteuzi wa wagombea litafanyika tarehe 8 Novemba, 2024 na viongozi wa vyama vya siasa wanatakiwa kuwasilisha ratiba ya mikutano ya kampeni tarehe 14 Novemba, 2024 na kampeni za uchaguzi zitafanyika tarehe 20 Novemba, 2024 hadi tarehe 26 Novemba, 2024.

Mhe. Mtambi amezitaja sifa za mpiga kuwa kuwa ni Raia wa Tanzania, mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, mkazi wa Mtaa, Kijiji, au Kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika, aliyejiandikisha kupiga kura katika Mtaa, Kijiji, au Kitongoji chake.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Uchaguzi Mkoa wa Mara Bwana Dominicus Lusasi amesema Mkoa wa Mara una jumla ya tarafa 20, kata 178, mitaa 242, vijiji 458 na vitongoji 2,502, Wilaya sita na Halmashauri tisa.

Bwana Lusasi amesema Mkoa wa Mara unatarajiwa kuwa na wapiga kura 1,111,963 kulingana na takwimu Sensa ya Watu na Makazi yam waka 2022 zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

Bwana Lusasi amesema wakati wa uchaguzi Mkoa utakuwa na vituo vya uandikishaji 2,854 ambapo kati ya hivyo vituo 1,782 vipo kwenye majengo ya umma na vituo 1,065 havipo kwenye majengo ya umma na mkoa unatarajia kuwa na vituo vya kupigia kura 3,053 hii ni kutokana na ongezeko la vituo kwenye Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Kauli Mbiu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 ni “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, wazee wa kimila na machifu, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, mashirika yasiyo ya kiserikali, waratibu wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.