• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi awapongeza wanamara kwa ukomavu wa kisiasa

Posted on: November 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepiga kura kuwachagua viongozi wa Serikali ya Mtaa katika kituo kilichopo Ofisi ya Kata Mukendo, Manispaa ya Musoma na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu wa kisiasa na kuwataka wajitokeze kwa wingi kupiga kura.

Akizungumza mara baada ya kupiga kura Mhe. Mtambi amesema katika kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa wananchi wameonyesha ukomavu wa kisiasa uliosababisha kampeni kufanyika kwa amani na utulivu na hamna malalamiko ya vyama au wagombea kufanyiwa fujo wakati wa kampeni.

“Ninawapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu mkubwa wa kisiasa waliouonyesha katika kipindi chote cha kampeni na ninawakumbusha kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amevitaka vyama vya siasa na wanachama wao kuheshimu na kuzifuata kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambazo walishiriki kuzitunga na kama kuna malalamiko yoyote wanaweza kuwasilisha malalamiko hayo sehemu zinazohusika kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima wakati huu wa uchaguzi na kuwataka wananchi kuhakikisha kuwa baada ya kupiga kura wanaenda kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Mhe. Mtambi amewaonya watu wanaopanga kufanya vurugu na kuahidi kuwa Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara na wananchi wa Mkoa wa Mara hawatamvumilia mtu yoyote atakayeanzisha fujo katika kipindi hiki na kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali itawachukulia hatua za kisheria watu wote wanaoanzisha vurugu wakati huu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka akizungumza katika eneo hilo amewaomba wananchi wa Wilaya ya Musoma kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi na kuwahakikishia usalama wao wakati wote wa uchaguzi.

Mhe. Chikoka pia amewataka wananchi kuachana na mikusanyiko isiyo ya lazima na kutoa taarifa kwa viongozi wanapohisi kuna uwezekano wa uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa mbili kamili asubuhi na vinategemewa kufungwa saa 10 jioni na baada ya kupiga kura wananchi wanashauriwa kuondoka katika eneo la kituo cha kupiga kura kwa utulivu na amani.

Leo ni siku ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo wananchi wanachagua viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa Mitaa/Vijiji, wajumbe wa serikali ya mtaa/kijijji, wenyeviti wa vitongoji na kauli mbiu ya mwaka huu ni Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.