• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi awahamasisha waandishi kuutangaza Mkoa wa Mara

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Mkoa wa Mara yaliyofanyika katika Hoteli ya Afrilux ,Manispaa ya Musoma na kuwataka Waandishi wa Habari kutumia maarifa yao na ubunifu kuutangaza Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kufunga maadhimisho hayo, Mhe. Mtambi amesema taswira ya Mkoa wa Mara iliyopo nje ya Mkoa ni tofauti na hali halisi iliyopo ndani ya Mkoa wa Mara na kwamba kuna mambo mengi mazuri yaliyopo lakini hayapewi kipaumbele na Waandishi wa Habari na vyombo vya habari hapa nchini.

“Mkoa wa Mara una mambo mengi mazuri ambayo hayaandikwi ipasavyo au hayaandikwi kabisa kama vile uwepo wa asilimia kubwa ya Ziwa Victoria, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, madini, wasomi na viongozi kutoka Mara, wakulima na wafugaji wazuri hayapewi kipaumbele kwenye vyombo vyetu vya habari” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amewataka Waandishi wa Habari kuandika habari kwa kuzingatia weledi na maadili ya uandishi wa habari na uhalisia uliopo na sio kutoa habari mbaya tu kila wakati ambazo amesema hazijengi taswira nzuri ya Mkoa wa Mara kwa wadau wake waliopo ndani na nje ya Mkoa wa Mara.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka Watendaji Wakuu wa Taasisi na Viongozi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa waandishi wa Habari ili waweze kupata taarifa kwa urahisi na kutekeleza kwa ufanisi  majukumu yao.

Kanali Mtambi ameipongeza Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri inayoifanya na kumuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kuitafutia kiwanja Klabu hiyo ili iweze kujenga ofisi na kuahidi kuwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara itachangia katika ujenzi wa ofisi ya Klabu hiyo.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka waandishi kutumia vizuri uhuru waliopewa na kuongeza kuwa pamoja na Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwapa uhuru wa kutosha, uhuru huo umeambatana na wajibu kwa Waandishi wa Habari kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, miongozo na taratibu za nchi.

Mkuu wa Mkoa pia amesema Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi wa Kata ya Nyatwali Wilaya ya Bunda wanahama katika eneo hilo kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA).

Akisoma risala ya Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara, Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo Bwana Raphael Okello amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa aliouonyesha kwa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara na hususan kushiriki katika maadhimisho hayo.

Bwana Okello ameeleza kuwa Klabu yao imeanza mchakato wa kutafuta kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi lakini inakabiliwa na uhaba wa fedha na kuiomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na wadau wengine kuwasaidia kununua kiwanja hicho.

Bwana Okello amezitaja baadhi ya changamoto kuwa ni baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali wamekuwa hawatoi ushirikiano kwa Waandishi wa Habari katika kutekeleza majukumu yao jambo ambalo linakiuka uhuru wa kujieleza na upatikanaji wa habari.

Ameitaja changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya Waandishi wa Habari kukosa bima ya afya na hivyo kuwawia vigumu kupata matibabu pindi wanapokuwa wameugua.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa pia na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Manispaa ya Musoma, Mgodi wa Barrick North Mara, Wakala wa Maji Vijijini na Mijini (RUWASA), Wakala wa Misitu (TFS), viongozi wa vyama vya siasa, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.  

Kitaifa Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yalifanyika Mkoani Dodoma tarehe 03 Mei, 2024 na Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (Mb.).

 Kauli mbiu ya maadhimisho haya mwaka huu ilikuwa “Uandishi wa Habari na Changamoto za Mabadiliko ya Tabia Nchi”.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.