• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi atoa siku saba Afisa Ardhi aliyehamishwa arudishwe Rorya

Posted on: May 31st, 2024

Mkuu wa Mkoa leo amefanya ziara katika Halmashauri ya Rorya na kuzungumza na wafanyakazi wa Halmashauri hiyo ambapo ametoa siku saba kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kumrejesha Bwana Fred Kijalawa Afisa Ardhi Mteule aliyehamishiwa Wilaya ya Serengeti kujibu hoja Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kumuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kumrejesha Bwana Kijalawa ili aisaidie Halmashauri kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusiana na fedha hizo.                

“DAS wasiliana na RAS mhakikishe huyu jamaa anarudi na anajibu hoja zote za ukaguzi kuhusiana na mradi huo ambao uliletewa fedha na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ndani ya siku saba” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mhe. Gerald Ng’ong’a ameeleza kuwa Halmashauri hiyo haipati ushirikiano wanaohitaji kutoka Idara ya Ardhi Wilaya ya Rorya ambayo imekuwa ikitekeleza miradi lakini haitoi taarifa kwenye Baraza la Madiwani.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa Idara hiyo ilipewa fedha za mkopo shilingi bilioni moja ambapo mpaka sasa hamna taarifa ya matumizi ya fedha hizo na kuna hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambazo hazina majibu kutokana na kukosa taarifa.

“Kwa niaba ya Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Rorya tunaomba utusaidie kwa kumrejesha Afisa Ardhi aliyehusika na matumizi ya fedha hizo ambaye baada ya hapo alihamishiwa Wilaa ya Serengeti na hatoi ushirikiano katika kujibu hoja tulizonazo” amesema Mhe. Ng’ong’a.

Mhe. Ng’ong’a ameeleza kuwa waliwahi kumuomba KamishnaMsaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara kusaidia kujibu hoja hizo lakini mpaka sasa hoja zipo na Halmashauri haina majibu ya kuridhisha kuhusiana na matumizi ya fedha hizo katika utekelezaji wa mradi huo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, kwa sasa Idara hiyo imepewa miradi mingine miwili na Baraza la Madiwani halijui gharama za mradi, wanufaika wa mradi, mradi utatekelezwa eneo gani na unamanufaa gani na kumekuwa hakuna ushirikishwaji katika utekelezaji wa miradi hiyo.

“Sisi kama Halmashauri tunataka tupate taarifa ya miradi yote ambayo inatekelezwa na Wizara au taasisi nyingine za umma katika Halmashauri yetu ili tuweze kuijua na kuisimamia miradi hiyo kwa manufaa ya wananchi” amesema Mhe. Ng’ong’a.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Juma Chikoka ameeleza kuwa Wilaya inaendelea kuwahamasisha wananchi kutunza mifugo yao kwa kujenga mazizi ya pamoja ili kudhibiti wizi wa mifugo katika Wilaya hiyo.

Mhe. Chikoka amewataka wananchi kuipa hadhi inayostahili mifugo yao ili kudhibiti wimbi wa wizi wa mifugo katika wilaya hiyo. 

Mhe. Chikoka ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya imeanza kukawakaribisha uwekezaji katika ufuvi na ufugaji wa samaki wa kisasa kwa njia ya visimba na kuongeza kuwa kwa sasa kuna visimba 72 vya wadau na vya Serikali katika Halmashauri hiyo. 

Mhe. Chikoka amesema kwa sasa Serikali inatekeleza Mradi wa Maji wa Rorya-Tarime ambapo serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 134 katika mradi huo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.