• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi ataka kasi Chuo cha VETA Burunga

Posted on: May 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ametembelea ujenzi wa Chuo cha Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) katika eneo la Burunga, Kata ya Uwanja wa Ndege na kutaka kasi ya ujenzi wa chuo hicho iongezeke ili ujenzi uweze kukamilika haraka.

Mhe. Mtambi pia amemtaka Mhandisi anayesimami mradi huo kuwepo eneo la mradi atakapokuja kukagua tena baada ya siku 14 ili atoe taarifa ya kitaalamu kwa nini mradi huo umechelewa kukamilika kinyume na maelekezo ya Serikali.

“Mimi nitakuja hapa baada ya siku 14 kuona maendeleo ya ujenzi, ninataka kuona mabadilko na majibu ya vifaa vinavyotakiwa kuletwa katika eneo la ujenzi na Wizara (Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia) ili tupate hatma ya ukamilishaji wa mradi huu” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mthibiti Ubora wa Wilaya ya Serengeti Bwana Nyoyo Andrea Nyangati ambaye ndio msimamizi wa mradi huo kwa niaba ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  amesema ujenzi huo ni awamu ya kwanza ya mradi huo na inahusisha majengo tisa (9) kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni moja.

Bwana Nyangati ameeleza kuwa kwa sasa ujenzi wa majengo hayo umefikia asilimia 47 na baadhi ya majengo ujenzi wake umesimama wakisubiria vifaa kutoka kwa wazabuni waliopewa zabuni na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Bwana Nyangati ameeleza kuwa mpaka sasa ujenzi huo umepokea jumla ya shilingi 345,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa maboma yote na kupandisha kuta za baadhi ya majengo ya Chuo hicho na majengo mengine kusubiria vifaa vya ujenzi kutoka Wizarani.

Bwana Nyangati ameeleza changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa mradi huo ni pamoja na mvua za vuli na masika zilizokuwa zinanyesha kuzuia upelekaji wa vifaa vya ujenzi katika eneo hilo, uhaba wa maji ambao ulitatuliwa kwa kujenga kisima kilichokusanya maji ya mvua.

Changamoto nyingine ni okosefu wa umeme katika eneo la mradi na kutokuwepo kwa barabara ya uhakika ya kufika katika eneo la mradi wa ujenzi na hivyo kukwamisha upelekaji wa vifaa na hususan wakati wa mvua za vuli na masika.

Chuo cha VETA ni sehemu ya vyuo vya VETA vinne vinavyoendelea kujengwa kwa awamu hii katika Mkoa wa Mara ambapo vingine vinajengwa katika Wilaya za Tarime, Rorya na Bunda huku Serikali ikiwa imekamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Wilaya ya Butiama mwaka 2022.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na baadhi ya Wajumbe wa Kamatiya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwenyekiti na Menejimenti ya Wilaya ya Serengeti na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, taasisi na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.