• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi ataka chakula kwa wanafunzi Sekondari ya Butuguri

Posted on: March 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 28 Machi, 2025 ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi katika Shule ya Sekondari ya Butuguri na kuutaka uongozi wa Wilaya kuhakikisha kuwa wanafunzi wa shule hiyo wanapata walau mlo mmoja wakiwa shuleni.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Nne wa shule hiyo na kumtaka Mkuu wa Wilaya kama wazazi watagoma kuchangia chakula kwa hiari wachukuliwe hatua za kisheria kuwawezesha wanafunzi waweze kusoma vizuri.

“Hili sio la kubembeleza, haya ni maamuzi ya Serikali kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi waweze kusoma vizuri, kama hawataki kuchangia kwa hiari wachukuliwe hatua” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mhe. Moses Kaegele kukutana na wazazi na walezi wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Butuguri ili kuweka mkakati wa kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo wanapata angalau mlo mmoja shuleni.

Aidha, ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuangalia uwezekano wa kuajiri walimu wa muda katika shule hiyo ili kukabiliana na upungufu wa walimu wa masomo ya Sanaa na lugha katika shule hiyo.

Akikagua mradi wa ujenzi wa mabweni na madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano katika shule hiyo, Mhe. Mtambi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kwa kuwabadilisha wakandarasi waliopewa zabuni ya kujenga mabweni na madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule hiyo.

“Ninawapongeza kwa kuwabadilisha wakandarasi waliopewa kazi ya kujenga mabweni na madarasa katika mradi huu na kuufanya mradi uendelee baada ya changamoto zilizokuwa zimejitokeza” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Mara kuacha kuutaja Mfumo wa Manunuzi ya Serikali (NEST) kama sababu ya kuchelewa kwa miradi na badala yake amezitaka kutoa mafunzo zaidi kuhusiana na matumizi ya mfumo huo kwa watendaji na wazabuni mbalimbali wanaohusika katika utekelezaji wa miradi ili wautumie mfumo vizuri.

“Changamoto kubwa ni watumiaji wa mfumo huu, Halmashauri toeni mafunzo kwa wazabuni ambao wanauwezo wa ktekeleza miradi na hawajaujua mfumo na maafisa wanaosimamia utekelezaji wa miradi ili kukabiliana na changamoto hiyo” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Butuguri Mwalimu Nyamtelele Christopher amesema Shule hiyo ilipokea shilingi 510,448,303.78 kutoka Serikali Kuu, SEQUIP, na EP4R kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa mabweni, madarasa na matundu ya vyoo kwa nyakati tofauti kuanzia tarehe 11 Juni, 2024.

Mwalimu Christopher amesema ujenzi wa madarasa na bweni moja na madarasa manne umekamilika huku ujenzi wa madarasa manne upo kwenye ukamilishaji, ujenzi wa bweni moja upo hatua ya kupandisha kuta wakati bweni linguine lipo hatua ya msingi na ujenzi wa matundu ya vyoo upo kwenye ukamilishaji.

Mwalimu Christopher amesema changamoto kubwa katika utekelezaji wa mradi huo ni matumizi ya mfumo wa NEST, kukosekana kwa maji eneo la mradi na mvua kubwa iliyoathiri upelekaji wa vifaa eneo la mradi.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama, baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi na maafisa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.