• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi asikiliza kero za wananchi

Posted on: July 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi katika utaratibu wake wa kawaida wa kusikiliza kero za wananchi siku ya Ijumaa, leo tarehe 5 Julai, 2024 amesekiliza kero za wananchi katika ukumbi wa uwekezaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kutoa maamuzi mbalimbali.

Mhe. Mtambi amemsikiliza Bibi Joyce Marwa Matiku (66) ambaye nyumba yake pamoja na shamba viliuzwa mwaka 2017 na mtoto wake wa kwanza Joseph Marwa Matiku (49) na kesi imeenda hadi mahakama kuu lakini haikuwa inapata maamuzi kutokana na makosa ya ufunguaji wa kesi kwa sababu hakuwa na wanasheria wa kumsimamia.

Katika maamuzi yake, Mhe. Mtambi amempatia mawakili watakaomsaidia kufungua upya kesi hiyo na kumueleza Bibi Matiku kuendelea kuishi katika nyumba hiyo iliyouzwa mpaka maamuzi ya Mahakama yatakavyotolewa baada ya kuwa amesimamiwa na mawakili aliompatia yatakapoamuru vinginevyo.

Mhe. Mtambi amewasilikiza wananchi wa Kijiji cha Bumangi, Wilaya ya Butiama ambao eneo lao walilopanga kujenga soko liligawiwa kwa makosa na dalali wa mahakama katika kesi ya talaka baina ya wanandoa wawili na eneo hilo kupewa mke wa wanandoa hao.

 Katika maamuzi yake, Mhe. Mtambi amewataka viongozi hao kuendelea kulitumia eneo lao lililogawiwa katika kesi ya talaka ya wanandoa hao na kama kuna mtu atakuja kuwaondoa wawataarifu viongozi wa Wilaya ya Butiama na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Kanali Mtambi amewasikiliza wananchi wanaoidai fidia Manispaa ya Musoma baada ya maeneo yao kutumika kujenga shule za Sekondari za kata na kuwataka kufika jumatatu tarehe 8 Julai, 2024 wakiwa na vielelezo vyao ambapo pia Mkurugenzi na baadhi ya maafisa kutoka Manispaa ya Musoma wataitwa kujibu hoja zao.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa kibali kwa mwananchi aliyekuwa na shamba katika eneo lililouzwa kwa Wakala wa Vipimo kwenda kukata miti yake iliyokuwa katika eneo hilo kabla halijauzwa kwa Wakala wa Vipimo.

Katika kusikiliza kero za wananchi, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Dominicus Lusasi, Kamati ya kusikiliza Kero za wananchi aliyoiunda na baadhi ya Maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.