• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi apongeza mpango wa mikopo kwa wajasiriamali

Posted on: October 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekutana na kuzungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Bwana Amon Anastaz Mpanju ambaye yupo Mkoani Mara kwa lengo la kuzungumza na wafanyabiashara wadogo wadogo kuhusiana na mikopo mipya kwa wajasiriamali itakayotolewa na Serikali kupitia Benki ya NMB.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi ameipongeza Serikali kwa kuanzisha mikopo kwa ajili ya wajasiriamali na kuongeza kuwa jambo hili limefika wakati muafaka kwa kuwa amekuwa akipokea maombi kutoka kwa wajasiriamali na hususan ambao walikuwa hawapewi mikopo inayotolewa na Halmashauri.

“Ninaipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita kuja na wazo hili, kuna kundi kubwa la wananchi ambao walikuwa hawawezi kupata mikopo ya Halmashauri lakini na wao sasa watanufaika na mikopo hii itakayotolewa na Serikali” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa wananchi kupata uhakika wa mikopo yenye riba nafuu, itawasaidia kuanzisha na kuendeleza biashara zao na kuachana na mikopo inayotolewa na taasisi ambazo hazijasajiriwa ambayo inawaumiza wajasiriamali.

Kwa upande wake, Bwana Mpanju amesema mpango wa Serikali kutoa mikopo upo katika hatua nzuri ambapo tayari Benki ya NMB imeshinda kwa ajili ya kutoa mikopo hiyo kwa riba ya asilimia  saba isiyoongezeka.

Bwana Mpanju amesema ili kunufaika na mikopo hiyo wajasiriamali wanatakiwa kuwa na vitambulisho vya wajasiriamali ili kuweza kutambulika shughuli wanazofanya na kuweza kunufaika na mikopo hiyo ya wajasiriamali.

Bwana Mpanju amesema vitambulisho vya wajasiriamali vinatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 17 Oktoba, 2024 katika Mkoa wa Arusha wakati utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali unatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba, 2024.

Bwana Mpanju ameeleza kuwa mikopo hii itawasaidia wajasiriamali kukuza mitaji yao kwa sababu haina kikomo cha kukopa kutegemeana na makubaliano yatakayofikiwa kati ya mjasiriamali na Benki ya NMB na wazo la mjasiriamali katika biashara anayotegemea kuifanya.

Bwana Mpanju pia amezungumza na wajasiriamali wa Wilaya ya Musoma katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara ambao amewataka viongozi wa wajasiriamali kuwahamasisha wajasiriamali kupata vitambulisho vya wajasiriamali vitakavyowasaidia kupata mikopo hiyo yenye riba nafuu.

Akiwa kwenye mazungumzo hayo, Bwana Mpanju ametolea ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizotolewa na wajasiriamali walioshiriki kikao hicho na kuwahamasisha kuwahamasisha wenzao kuchukua kadi za wajasiriamali.

Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na maafisa kutoka Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.   

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.