• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi ampokea Meja Jenerali Gaguti

Posted on: February 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 18/2/2025 amempokea na kuzungumza na Mkuu wa Utumishi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Meja Jenerali Marco Gaguti na ujumbe wake waliopo katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika mapokezi hayo yaliyofanyika ofisini kwake, Mhe. Mtambi amesema hali ya usalama ya Mkoa wa Mara ni shwari na wananchi wanaendelea kufanya shughuli zao za kawaida za maendeleo.

Mhe. Mtambi amelipongeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kazi nzuri wanayoifanya kulinda amani na usalama wa nchi na hususan katika maeneo ya mipaka ya Tanzania.

Mhe. Mtambi amelishukuru JWTZ kwa ushirikiano wanaoutoa kwa Serikali ya Mkoa na kuahidi kuwa viongozi na Kamati ya Usalama ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano kwa JWTZ katika utekelezaji wa majukumu yao katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Meja Jenerali Gaguti akizungumza katika mapokezi hayo amempongeza  Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Usalama ya Mkoa kwa kuhakikisha hali ya amani na utulivu inakuwepo katika Mkoa wa Mara jambo ambalo amesema linawawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kujiletea kimaendeleo.

“Kutokana na amani na utulivu uliopo, wananchi wanaendelea kufanya shughuli zao za kujiletea maendeleo bila ya kuwa na hofu ya aina yoyote ile” amesema Meja Jenerali Gaguti.

Meja Jenerali Gaguti amemshukuru Mkuu wa Mkoa na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano wanaoutoa katika jeshi hilo 

Meja Jenerali Gaguti na ujumbe wake wapo katika ziara ya kawaida ya kikazi kwa siku mbili katika Mkoa wa Mara kuanzia leo na akiwa katika ziara hiyo ameambtana na maafisa mbalimbali kutoka makao makuu ya JWTZ.

Mapokezi hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Mshauri wa Mgambo wa Mkoa wa Mara, Mkuu wa Kikosi cha JKT Rwamkoma, Mkuu wa Kambi ya JWTZ Makoko.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.