• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi akabidhi magari RUWASA

Posted on: September 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza hafla fupi ya kukabidhi magari mawili yaliyotolewa na Serikali kwa ajili ya Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mara yatakayotumika katika Wilaya za Tarime na Serengeti.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo, Mhe. Mtambi amewataka watendaji wa RUWASA waliokabidhiwa magari hayo kuhakikisha kuwa magari hayo yanatumika vizuri na yawawaongezea kasi ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

“Kwa sasa RUWASA Mkoa wa Mara mna jumla ya magari matano ukijumlisha na magari matatu yaliyokuwepo na pikipiki 35, ni matumaini yangu kuwa magari haya yatatumika kuboresha huduma za upatikanaji wa maji kwa wananchi” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, ameitaka Mhe. Mtambi amesema RUWASA imepanga kununua pikipiki 25 ili kuimarisha suala la usafiri kwa wataalamu katika kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Mara.

Kanali Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya kusimamia matumizi ya magari hayo ili yadumu kwa muda mrefu na yatumike kutoa huduma kwa wananchi wa Wilaya hizo.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Mara Mhandisi Tulimpoki Mwakalukwa ameishukuru Serikali kwa kutoa magari hayo ambayo amesema walikuwa wanayahitaji sana kama kitendea kazi muhimu.

Mhandishi Mwakalukwa amesema tayari Serikali ilileta amagari mengine matatu ambayo yaligawiwa kwa Ofisi ya RUWASA Mkoa wa Mara, Wilaya ya Butiama na Wilaya ya Bunda wakati gari zilizokabidhiwa leo ni kwa ajili ya Wilaya ya Serengeti na Wilaya ya Tarime.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mwakalukwa, kwa sasa Wilaya ambazo hazina magari ni Musoma na Rorya ambayo yameshaombwa Serikalini.

Mhandisi Mwakalukwa amemshukuru Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso kwa kuidhinisha manunuzi na kuugawia Mkoa wa Mara magari hayo ambayo ameahidi kuyasimamia kwa ukaribu katika matumizi yake.

Kwa upande wake, Mhandisi wa RUWASA Wilaya ya Tarime Mhandisi Malando Mashapu ameipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vitendea kazi muhimu kwa RUWASA Wilaya ya Tarime.

Mhandisi Mashepu ameahidi kuwa magari hayo yatawasaidia katika kuwafikia wananchi katika maeneo yao na kuhakikisha wanapata maji na kutatua changamoto za maji kwa wakati.

Hafla ya kukabidhi magari hayo imehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Maafisa wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, RUWASA na Halmashauri za Mkoa wa Mara.   

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.