• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mtambi aagiza RUWASA kurejesha maji bure Nyamikoma B

Posted on: June 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameshiriki kikao maalum cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kuiagiza Mamlaka ya Maji Vijijini (RUWASA) kupeleka maji bure Shule ya Msingi Nyamikoma B iliyopo katika eneo la Pida, Wilaya ya Butiama.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya wananchi kuwasilisha malalamiko kuhusu RUWASA kukitumia kisima cha shule hiyo kilichochimbwa kwa ufadhili wa Shirika la PCI shuleni hapo na kuyasambaza katika eneo hilo na kuidai shule hiyo kulipa bili za maji kama watu na taasisi zilizopo katika eneo hilo.

“Naagiza maji kwenye shule hii yaletwe haraka na watatumia bure kwa sababu kisima hiki ni cha kwao kilichimbwa na mfadhili wao ili watoto waweze kupata maji kiurahisi, hamna kuwaletea bili za maji” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameagiza kuwa kwa kuwa shule hiyo imetoa kisima chake bure na kuruhusu maji yake yasambazwe kwa wananchi wa maoneo hayo, RUWASA itumie busara kurudisha huduma za maji katika shule hiyo haraka iwezekanavyo.

Mhe. Mtambi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Butiama kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo na kufuatilia pampu zilizokuwa zimefungwa katika kisima hicho ambazo RUWASA wanadai waliikabidhi kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo na Mwalimu Mkuu anadai ipo RUWASA.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bibi Eunice Makere ameeleza kuwa alipokea malalamiko hayo kutoka katika shule hiyo na kufanya kikao na RUWASA, uongozi wa Kijiji na uongozi wa watumia maji na kubaliana maji hayo yarejeshwe kabla shule hazijafunguliwa.

Bibi Makere amesema hata hivyo baada ya maji hayo kuunganishwa katika tanki lililojengwa na RUWASA na shule kutakiwa kulipia maji wanayoyatumia, shule hiyo haijaweza kulipia maji hayo na wanafunzi wa shule hiyo wamekosa maji kutokana na maamuzi hayo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Butiama Mhe. Christopher Marwa Siagi amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa michango yake aliyoitoa katika Baraza hilo maalum inayolenga kuleta tija.

Mhe. Siagi amemuomba Mkuu wa Mkoa kusaidia Shule ya Sekondari ya Mkono iliyopo katika Wilaya ya Butiama kupata maji kutokana na shule hiyo kuwa na wanafunzi wengi na kukosa maji ya uhakika ya kutumia.

Aidha, Mhe. Siagi ameitaka Halmashauri hiyo kutoa taarifa za fedha za miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo pindi fedha zinapoingia ili kukiwezesha Chama cha Mapinduzi kufanya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa kutokana na fedha hizo.

Kikao cha Baraza la Madiwani kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama, Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Hamashauri ya Wilaya ya Butiama.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.