• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Msovela Awataka Wakandarasi kukamilisha miradi kwa wakati

Posted on: July 30th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewataka wakandarasi waliopata zabuni za kutekeleza miradi ya Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) katika Mkoa wa Mara kukamilisha ujenzi wa barabara hizo kwa wakati.

Bwana Msovela ametoa maagizo hayo leo tarehe 30 Julai 2021 katika hafla ya kusaini mikataba na wakandarasi 122 waliopewa zabuni za kutengeneza barabara, vivuko na madaraja katika wilaya zote za Mkoa wa Mara.

“Niwaombe wakandarasi tujitahidi kukamilisha barabara hizi kwa wakati ili wananchi waweze kupata urahisi wa kusafiri na kusafirisha mizigo yao ikiwemo mazao yao kwa wakati” alisema Bwana Msovela.

Aidha amewataka wakandarasi kulipa tozo zozote za kisheria kwa halmashauri na mamlaka nyingine za serikali kwa wakati ili waweze kuendelea kufanya kazi zao vizuri bila kusmbuliwa.

Katibu Tawala pia amewakumbusha wakandarasi kutekeleza matakwa ya sheria za mazingira wakati wa ujenzi wa barabara hizo ili kuleta maendeleo endelevu ya Mkoa wa Mara.

Bwana Msovela amewaagiza wakandarasi hao kuajiri vibarua katika kazi za ujenzi kwenye miradi huo kutoka maeneo wanayojenga barabara hizo ili wananchi waweze kupata ajira na serikali ipate walinzi wa barabara zake.

Ameitaka TARURA kuimarisha usimamizi na kuhakikisha kuwa barabara hizo zinakamilika kwa wakati, kwa viwango vilivyokubalika na ubora unaoridhisha kwa mujibu wa mikataba.

“Mkisimamia kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni barabara hizi zitakamilika kwa ubora na katika muda uliopangwa kwa mujibu wa mkataba” alisema Bwana Msovela.   

Bwana Msovela ameziomba taasisi za fedha kuongeza ushirikiano wa kibiashara na wakandarasi hao ili barabara za Mkoa wa Mara ziweze kukamilika kwa wakati.

Ameelezea matumaini yake kuwa baada ya kukamilika kwa barabara hizi zitaenda kuufungua Mkoa wa Mara kimawasiliano na kurahisisha usafiri kwa wananchi.  

Kwa upande wake akizungumza katika ufunguzi wa hafla hiyo Mratibu wa TARURA  Mkoa wa Mara Mhandisi Musa Z. Mzimbiri ameeleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 8 kwa ajili ya kujenga barabara, vivuko na madaraja katika Mkoa wa Mara.

“Serikali pia imetenga zaidi shilingi bilioni 13.4 kwa ajili ya barabara za majimbo 10 ya uchaguzi ya Mkoa wa Mara katika kutekeleza miradi ya barabara za majimbo ya uchaguzi” amesema Mhandisi Mzimbiri.

Mhandisi Mzimbiri ameeleza kuwa miradi ambayo imewekwa saini leo ni miradi 122 inayotekelezwa na wazabuni 34 yenye gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 6.044 katika halmashauri na wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Hafla fupi ya kutia saini ya ujenzi wa barabara zinazosimamiwa na TARURA ilihudhuriwa pia na viongozi wa taasisi za kifedha, bima, madini, wakandarasi, maafisa kutoka Ofisi ya Mratibu wa TARURA Mkoa wa Mara na waandishi wa habari.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.