• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Msovela aendelea na ukaguzi wa Miradi

Posted on: November 9th, 2021

MSOVELA AFANYA UKAGUZI WILAYA TATU

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela leo tarehe 6 Novemba 2021 ameendelea na ukaguzi wa miradi kwa kufanya ukaguzi katika Wilaya nne wa ofisi za Maafisa Tarafa na pamoja na miradi miundombinu inayoendelea kujengwa kutokana na fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Akizungumza katika maeneo mbalimbali Bwana Msovela amewakumbusha wasimamizi wa miradi kuwa Mkoa wa Mara umeazimia kukamilisha miradi hiyo tarehe 1 Desemba 2021 ili kuruhusu wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanza masomo kwa wakati.

“Kama Mkuu wa Mkoa alivyoagiza, miradi hii tunapaswa kuikamilisha kabla ya muda uliopangwa na serikali,na hili tukiongeza juhudi inawezekana lengo hilo likatimia kwa wakati” alisema Bwana Msovela.

Katika miundombinu inayojengwa, Bwana Msovela ameshuhudia miundombinu ikiwa katika hatua mbalimbali za kujenga msingi na kuwataka Wasimamizi wa Kata kutoka Halmashauri kwenda kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa.

Aidha kutokana na uchakavu wa Ofisi za Maafisa Tarafa, Bwana Msovela aliagiza kuwa fedha za ukarabati wa majengo hayo zitengwe katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ili yaweze kukarabatiwa.

Aidha alisema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara itaangalia uwezekano wa kununua samani za ofisi na vitendea kazi kwa ajili ya Maafisa Tarafa wa Mkoa mzima.  

Katika ziara hiyo, Bwana Msovela alikagua Ofisi ya Afisa Tarafa ya Suba, Shule ya Sekondari ya Suba, Shule ya Sekondari ya Buturi, Shule ya Sekondari ya Pasta Raphael Odunga na Ofisi ya Afisa Tarafa Luo Imbo katika Wilaya ya Rorya.

Katika Wilaya ya Tarime alikagua Ofisi ya Afisa Tarafa ya Inano na Ofisi ya Afisa Tarafa ya Inchage. Katika Wilaya ya Serengeti Katibu Tawala alitembelea Ofisi ya Afisa Tarafa ya Ikorongo, nyumba iliyojengwa kwa ajili ya Afisa Tarafa ambayo haijapokelewa na Serikali baada ya kujengwa chini ya kiwango, Kituo cha Afya Kenyana na Shule ya Sekondari ya Samoche.

Katika Wilaya ya Butiama, Katibu Tawala alitembelea Ofisi na nyumba ya kuishi Afisa Tarafa ya Kiagata, Shule ya Sekondari ya Bumangi na Ofisi ya Afisa Tarafa ya Makongoro.

Bwana Msovela aliambatana na Kaimu Mhasibu Mkuu wa Mkoa Bwana Pascal Kajuna, Mkaguzi Mkuu wa Ndani Bwana Yusuf Luhende, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi- Miundombinu Mhandisi Richard Moshi, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi- Utawala na Rasilimaliwatu Bwana Dominicus Lusasi na Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara Bwana Fidel Baragaye.

Ziara hiyo ni mwendelezo wa ziara za Katibu Tawala kukagua miradi Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.