• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mpango wa M-Mama watambulishwa Mara

Posted on: February 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo ameongoza kikao cha utambulisho wa Mpango wa M-Mama katika Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao katika maandalizi na utekelezaji wa Mpango huu ili kuboresha utoaji wa huduma za afya ya Mama na Mtoto.

“Kinachohitajika hapa ni viongozi na watendaji wote kutimiza wajibu wetu ili kufanikisha maandalizi na hatimaye utekelezaji wa mpango huu katika Mkoa wa wetu ili kuokoa wanawake wajawazito na watoto wachanga” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango wa M-Mama katika bajeti zao za mwaka wa fedha 2023/2024 pamoja na kufanya maandalizi mengine yanayohitajika ili mpango uweze kuanza mwezi Mei, 2023 katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa Mpango wa M-Mama utawezesha upatikanaji wa usafiri wa kwenda katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa watoto changa na wanawake wajawazito katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto Mkoa wa Mara Bibi Leah Daniel ameeleza kuwa kwa sasa upatikanaji wa huduma za afya ya mama na mtoto katika Mkoa wa Mara umeimarika na Mkoa umefanikiwa kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga wanaofariki.

“Kwa sasa Mkoa una vituo vya kutolea huduma za afya 335 kutoka vituo 290 mwaka 2017 na vituo hivi vyote vinatoa huduma za mama na mtoto” amesema Bibi Leah.

Bibi Leah ameongeza kuwa kati ya vituo vyote vilivyopo, vituo 35 vinauwezo wa kufanya upasuaji na kuongeza damu kwa wagonjwa huku magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) zikiwa 13 tu kwa Mkoa mzima.

Kwa mujibu wa Bibi Leah, kuanza kwa Mpango wa M-Mama utasaidia kuokoa maisha ya wanawake wajawazito na watoto wachanga baada ya kuanza utekelezaji wake kwani wananchi watapata uhakika wa usafiri wa kwenda katika vituo vya kutolea huduma kwa kundi hilo maalum.

Bibi Leah ameeleza kuwa takwimu za mwaka 2022 zinaonyesha kuwa wajawazito 93,539 walijifungua katika vituo vya kutolea huduma, 344 walijifungua majumbani bila usaidizi wowote na wajawazito 131 walijifungua katika jamii kwa usaidizi wa wakunga wa jadi.

“Wengi wa wajawazito walioshindwa kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya ni kwa sababu ya kukosekana au kushindwa kumudu gharama za usafiri na hivyo kulazimika kuhatarisha maisha ya akina mama hawa” amesema Bibi Leah.

Usafiri utakaotumika kuwapeleka wajawazito na watoto vituoni ni magari, boti na meli za Serikali na watu binafsi kulingana na uhitaji wa eneo husika vitakavyokuwa vimesajiriwa na Halmashauri husika kwa ajili ya kutoa huduma hizo katika ngazi ya jamii.

 Mpango wa M-Mama ilizinduliwa rasmi na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 09 Desemba, 2023 mkoani Dodoma na kuagiza kusambazwa kwa mpango huo katika mikoa yote hapa nchini.

Awali kabla ya uzinduzi rasmi, Mpango huu umefanyiwa majaribio katika Mkoa wa Shinyanga na baadhi ya Wilaya za Mkoa wa Mwanza na Serikali imejiridhisha kuhusu manufaa ya mpango huu katika kuimarisha afya ya mama na mtoto.

Kikao cha utambulisho wa M-Mama kimehudhuriwa na Dkt. Yahya Hussein kutoka Ofisi ya Rais- Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bibi Rahma Bajir, Mkuu wa Kitengo cha M-Mama, Vodafone Foundation na watumishi wengine.

Aidha, utambulisho huo umehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meya na Wenyeviti wa Halmashaur za Mkoa wa Mara, Makaimu Wakurugenzi wa Halmashauri na Waganga Wakuu wa Halmashauri.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.