• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mkuu wa Mkoa apokea madarasa 58 Serengeti

Posted on: January 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amepokea vyumba vya madarasa 58, viti na meza kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.16 kwa ajili ya madarasa ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023.

Akizungumza baada ya kupokea madarasa hayo, Mheshimiwa Mzee ameipongeza Wilaya ya Serengeti kwa kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa ubora na kwa wakati.

“Ninawapongeza wote waliohusika katika usimamizi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa haya, kazi iliyofanyika ni nzuri na nimeridhika na ujenzi huu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee pia amezipongeza shule ambazo zimepanda miti kuzunguka maeneo yao na kuzitaka shule hizo kuongeza miti zaidi ili kila mwanafunzi aweze kupata mti wake wa kuuhudumia akiwa shuleni hapo.

Hata hivyo, Mheshimiwa Mzee ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kusimamia na kuhakikisha mapungufu madogo madogo yaliyobainika yanaondolewa ili wanafunzi wanapoanza masomo mapungufu hayo yawe yameondolewa.

Mapungufu hayo ni pamoja na ubora wa viti na meza zilizotengenezwa, uingizaji wa umeme katika vyumba vya madarasa, uwekaji wa ngazi katika madarasa hayo na kufanya landscaping katika maeneo ya shule hizo.

Aidha, Mheshimiwa Mzee ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuongeza vyumba vya madarasa katika shule za sekondari za Mugumu na Rigicha ambazo zilieleza kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa kutokana na uwingi wa wanafunzi katika shule hizo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Dkt. Vincent Mashinji ameeleza kuwa kukamilika kwa vyumba hivyo vya madarasa kutawasaidia wanafunzi zaidi ya 7,000 wanaoanza kidato cha kwanza mwaka huu.

“Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Serengeti, ninamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kujenga vyumba 58 vya madarasa katika Wilaya ya Serengeti vimesaidia sana katika maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza” alisema Dkt. Mashinji.

Mheshimiwa Dkt. Mashinji amewataka wazazi wa wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kuhakikisha kuwa wanapeleka watoto wao shule kwa hiari yao, wakishindwa kufanya hivyo, Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria.

Aidha, amewaagiza watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata kuhakikisha wazazi wote wenye watoto wanaotakiwa kwenda shule wanapelekwa shule ili watoto waweze kupata haki yao ya kusoma na kujifunza kulingana na umri wao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Mrobanda Japan Mkoma ameeleza kuwa CCM imefurahishwa na kazi nzuri iliyofanyika ya ujenzi wa madarasa hayo ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama hicho.

Mheshimiwa Mrobanda amewataka watendaji wote kuendelea kutekeleza Ilani kwa nguvu ili wananchi waweze kukuelewa na kukipenda Chama cha Mapinduzi na viongozi wake.

Aidha, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa na kutoa nafasi kwa wanafunzi wengi kuweza kusoma.  

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa amekagua Shule ya Sekondari ya Rigicha (vyumba 4), Shule ya Sekondari ya Natta (chumba kimoja), Shule ya Sekondari ya Makundusi (vyumba 3), Shule ya Sekondari Mugumu (vyumba 8) na Shule ya Sekondari ya Mapinduzi (vyumba 10).

Katika ziara hiyo pia, Mkuu wa Mkoa amepata nafasi ya kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Natta na kusikiliza maoni, kero, changamoto zinazowakabili na kuzitolea ufafanuzi na mrejesho.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu, watumishi wengine kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, viongozi wa CCM Wilaya ya Serengeti, Madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.