• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Milioni 720 kuboresha huduma ya maji Komuge

Posted on: February 29th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) leo ameendelea na ziara yake katika Wilaya za Rorya na Butiama ambapo ametembelea mradi wa maji Komuge na kuahidi kutoa shilingi milioni 720 kwa ajili ya kuboresha mradi wa maji Komuge.

Serikali imetoa ahadi hiyo baada ya kusikiliza maombi ya wananchi, Mbunge wa Jimbo la Rorya Mhe Jaffari Chege na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe. Agness Marwa ambao wameomba mradi huo uboreshwe ili wananchi waweze kupata huduma.

Akizungumza na wananchi wa eneo la Komuge Mhe. Majaliwa amesistiza adhma ya Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua mama ndoo kichwani na kuleta mahitaji mengine ya msingi kwa Watanzania.

 Mhe. Majaliwa ameitaka RUWASA kukamilisha maboresho ya mradi huo kwa wakati ili wananchi waweze kupata maji ya uhakika.

Wakati huo huo, Mhe. Waziri Mkuu ametoa wiki moja kwa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kukamilisha uchunguzi wa mwalimu wa Shule ya Msingi Kinesi B  ambaye anatuhumiwa kuiba vifaa na fedha za ujenzi wa shule.

“Shule hiyo ilipewa shilingi milioni 540 hapa haijakamilika kwa sababu vifaa na fedha taslimu shilingi milioni 24 vimeibiwa na mwalimu huyo

Mhe. Waziri Mkuu amevitaja vifaa vilivyoibiwa kuwa ni pamoja na mlango wa chuma, saruji mifuko 100, mabati 80, feni 50, gypsum board 20, ndoo za rangi zenye thamani ya milioni 11, kokoto na nyaya za umeme.

Mhe. Waziri Mkuu amesema Mwalimu huyo amesababisha madeni ya shilingi milioni 9 kwa fundi wa ujenzi Victor Joseph John jambo ambalo amesema halikubaliki kwa watumishi wa umma kuchukua kiholela fedha na mali walizokabidhiwa kuzitunza.

“Watumishi wasio waadilifu wanawachafua wenzao, wanarudisha nyuma jitihada za Serikali na kukwamisha maendeleo ya wananchi, hawapaswi kuvumiliwa hata kidogo, hii ni hujuma” amesema Mhe. Majaliwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rorya Bwana Abdul Mtaka ameeleza kuwa walimtaka mwalimu atoe maelezo kwa maandishi kwa nini ameshindwa kusimamia huo mradi na kusababisha hasara, Mwalimu alileta majibu yake na kwa sasa wanaendelea na kumchukulia hatua za kinidhamu.

“Tulibaini wizi huo baada ya kupata taarifa ya Mkaguzi wa Ndani na suala hilo, kwa sasa tunasubiria matokeo ya uchunguzi wa TAKUKURU ulioanza Novemba, 2023” amesema Bwana Mtaka.

Katika Wilaya ya Rorya, Mhe. Waziri Mkuu ametembelea Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, amefanya mkutano wa hadhara na wananchi eneo la Utegi na kuelekea Wilaya ya Tarime ambapo amefanya mkutano wa hadhara katika eneo la Sirari, kuweka jiwe la msingi katika mradi wa soko la kimkakati la Halmashauri ya Mji wa Tarime kabla ya kuhitimisha ziara yake kwa kufanya mkutano wa hadhara katika Mji wa Tarime.

 Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Mkuu ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini, Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Deo Ndenjembi na Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.