• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mhe. Sulumbu awataka wafugaji kufuga kisasa

Posted on: July 4th, 2024

Mwakilishi wa Mkuuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Maulid Sulumbu leo amefunga rasmi mashindano ya Nyama Choma Festival Wilaya ya Tarime yaliyofanyika katika mnada wa Mtana, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kuwataka wafugaji wa Mkoa wa Mara kufanya ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija katika ufugaji wao.

Mhe. Sulumbu amesema hayo alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi katika ufungaji wa mashindano ya Nyama Choma Festival na kuwahimiza wafugaji kuchangamkia fursa inayoletwa na mashindano hayo katika Mkoa wa Mara.

“Lengo la kuanzisha mashindano haya ni kutangaza fursa zinazopatikana katika Mkoa wa Mara na hususan uwepo wa mifugo mingi ambayo ina nyama bora kutokana na aina ya mbegu ya mifugo na ufugaji unaofanyika katika Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Sulumbu.

Mhe. Sulumbu amewahimiza wawekezaji kuja kuwekeza katika viwanda vya kusindika nyama, ngozi na mazao mengine ya mifugo katika Mkoa wa Mara ili kutoa soko la uhakika kwa wafugaji na wachuuzi wa mifugo wa Mkoa wa Mara.

Kanali Sulumbu ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, amechukua fursa hiyo kuwashukuru washiriki wa mashindano na wadhamini wa mashindano hayo kwa kujitokeza kwao kufanikisha Nyama Choma Festival katika Wilaya ya Tarime.  

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa majaji katika mashindano hayo Bwana Gambaless Timotheo amesema washiri wa mashindano hayo walikuwa sita na amemtaja mshindi wa mashindano hayo kuwa ni Charles Joseph Mniko maarufu kama Chale Nyama ambaye amejishindia shilingi 500,000.

Bwana Timotheo amemtaja mshindi wa pili kuwa ni Bwana Christopher maarufu kama Miti Mirefu ambaye ameshinda shilingi 300,000 huku Mombasa Nyamachoma akiwa mshindi wa tatu ambaye ameshinda shilingi 200,000.

Bwana Timotheo amewataja washiriki wengine walioshiriki mashindano hayo kuwa ni Rajusa Trading and food points aliyeshika nafasi ya nne; Peter Okinda nafasi ya tano wakati Emmanuel Siguda ameshika nafasi ya sita na kuwapongeza washiriki wote kwa kazi kubwa waliyoifanya.

Bwana Timotheo amevitaja vigezo vya washindi kuwa ni pamoja na kusajiriwa kama mshiriki wa mashindano, usafi wa mazingira, usafiri binafsi wa wapishi, ubora wa nyama na vikolombwezo vya kwenye nyama kama vile pilipili, kachumbari na huduma kwa wateja.  

Kwa upande wake, mshindi wa mashindano hayo Bwana Charles Joseph Mniko amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuanzisha mashindano hayo ambayo amesema ni mara ya kwanza kufanyika mashindnao ya kuchoma nyama katika Wilaya ya Tarime.

Bwana Mniko amesema amekuwa katika biashara ya kuchoma nyama kwa miaka 30 sasa lakini hakuwahi kushiriki katika mashindano kama hayo na anawashukuru waandaaji kwa kuanzisha fursa nzuri kwa wafanyabiashara kupanua uzoefu wao.

Bwana Mniko amewaomba waandaaji kuendelea kuandaa mashindano mengine kama hayo katika Wilaya ya Tarime ilikutoa fursa kwa wachoma nyama wengi zaidi kujitokeza na kuleta ushindani ambao utaboresha biashara yao.

Mashindano hayo yamehudhuriwa pia na viongozi wa Halmashauri za Wilaya ya Tarime, Wakurugenzi wa Tarime TC, Tarime DC, Bunda TC, Butiama DC na Rorya DC  maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Halmashauri za Mji wa Tarime na Wilaya ya Tarime na Halmashauri nyingine za Mkoa wa Mara.

Hii ni mara ya pili kwa Nyama Choma Festival kufanyika katika Mkoa wa Mara baada ya kufunguliwa katika mnada wa Kiabakari, Butiama na mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika pia kesho tarehe 4 Julai, 2024 Wilaya ya Musoma katika stendi ya mabasi ya Bweri.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.