• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mhe. Silinde aipongeza Tarime DC na Mji wa Bunda

Posted on: December 5th, 2022

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa Mhe. David Ernest Silinde leo amehitimisha ziara yake Mkoa wa Mara kwa kuzipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kwa kazi nzuri ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Mheshimiwa Silinde ametoa pongezi hizo katika maeneo tofauti tofauti baada ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mheshimiwa Silinde ametembelea Shule ya Sekondari ya Nyabisaga (madarasa 3), Shule ya Sekondari ya Nyantira (madarasa 2), na Shule ya Sekondari ya Kemambo (darasa 1) yote yakiwa katika hatua za ukamilishaji.

Mheshimiwa Silinde akiwa katika Shule ya Sekondari ya Kemambo amemtaka Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara kutoa motisha kwa Shule ya Sekondari ya Kemambo kwa kukamilisha mapema ujenzi wa madarasa ambapo Waziri alikuta mafundi wakiendelea kufanya usafi baada ya kazi ya ujenzi kukamilika.

Katika Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mheshimiwa Silinde ametembelea Shule ya Sekondari ya Nyamisangura ambayo awali ilipewa fedha za kujenga vyumba 11 vya madarasa, lakini baadaye vyumba vitano kati ya hivyo vilihamishiwa katika Shule ya Sekondari ya Turwa B na shule hiyo kubaki na vyumba sita vya madarasa.

Hata hivyo, vyumba vitatu vilikuwa kwenye uezekaji wakati vyumba vitatu vingine vikiwa kwenye lenta jambo ambalo halikumfurahisha Mheshimiwa Naibu Waziri.  

Naibu Waziri pia alitembelea Shule ya Sekondari ya Bunda (madarasa 3) na Shule ya Sekondari ya Nyamikokoto ambayo inajengwa mpya kupitia mradi wa SEQUIP katika Kata ya Bunda Stoo ambayo itachukua wanafunzi wa Kata ya Bunda Mji na Kata ya Bunda Stoo.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri aliambatana na Wakuu wa Wilaya za Tarime na Bunda, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala Wasaidizi Sehemu ya Elimu na Sehemu ya Miundombinu, Mbunge wa Tarime Vijijini, Wenyeviti na Wakurugenzi wa Halmashauri, watumishi wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.