• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yazungumza na viongozi wa Dini

Posted on: April 17th, 2020

16 Aprili 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima leo amefanya mazungumzo na viongozi wa madhehebu na jumuiya mbalimbali za kidini wanaofanya shughuli zao katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kikao na viongozi hao Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa Tanzania na ulimwengu wote tupo katika mapambano makubwa dhidi ya janga la homa ya mapafu inayosababishwa na  virusi vya Corona maarufu kama COVID 19.

“Leo tumewaita hapa kutokana na umuhimu wenu katika masuala ya kiimani mnayoyaongoza katika jamii inayowazunguka” alisema Malima.

Alieleza kuwa pamoja na mambo mengine viongozi wa Mkoa wa Mara wanatarajia viongozi wa dini pamoja na kuliombea taifa, wasaidie katika juhudi za kupambana na ugonjwa wa Corona hapa nchini na hususan kwa wananchi wanaowahudumia.

“Ninawashukuru sana viongozi wote wa dini kwa maombi yenu ya kuliombea taifa hili mnayoendelea nayo, tunaendelea kumwomba Mungu atusikie kilio chetu” alisema Mheshimiwa Malima.

Akizungumza katika mkutano huu, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga ameeleza kuwa viongozi wa dini wanatakiwa kuendelea kupata elimu sahihi ya corona na kuisambaza kwa waumini wao ili kuwakinga na janga la corona.

Dkt. Tinuga amewataka viongozi hao kubuni njia mbalimbali za kuwaelimisha waumini ikiwa ni pamoja na nyimbo na kuonyesha mifano ya namna ya kujikinga na corona.

“Itakuwa vizuri kama kwenye kila ibada au swala, waumini wakapata nafasi hata ya dakika 10 kuambiwa habari za janga la Corona na namna ya kujikinga.

Kwa upande wake Askofu Michael Msoganzila wa Jimbo Katoliki Musoma alieleza kuwa kutokana na janga hili kanisa hilo limebadilisha sana namna ya kuendesha misa na kupunguza baadhi ya vitu ambavyo sio vya lazima.

Aidha Kanisa limetunga sala ambayo husaliwa katika kila familia kuliombea taifa na waumini wote na kumuomba Mungu aliepushe taifa katika janga la Corona.

“Hata hivyo kuna taasisi za elimu ambazo zinamilikiwa na taasisi ya dini ambazo kutokana na athari ya majanga ya corona itakuwa ngumu kuwalipa wafanyakazi wao mishahara hususan kama janga hili litaendele kwa muda mrefu” alisema Mloganzila

Kwa upande wake Shehe Mkuu wa Mkoa wa Mara Bwana Sheikh Msabaha Kassimu ameeleza kuwa anashukuru kuwa serikali imeruhusu masuala ya dini yaendelee wakati huu, na wao wanachukua tahadhari zote za kujikinga na corona.

 Katika mkutano huo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, maafisa waandamizi na wataalamu mbalimbali wa afya.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.