• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yazindua utekelezaji wa anuani za makazi

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amezindua utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuhusu anuani za makazi.

Mheshimiwa Hapi amezindua utekelezaji huo leo katika ukumbi wa uwekezaji ambapo ametoa mwisho wa utekelezaji wa mradi huo kwa Mkoa wa Mara kuwa tarehe 1 Aprili 2022.

“Mheshimiwa Rais katika maelekezo yake amesema mwisho wa kutekeleza jambo hili kitaifa ni tarehe 1 Mei, 2022 lakini sisi kwa Mkoa wa Mara mwisho ni tarehe 1 Aprili 2022 ili kutoa nafasi ya tathmini na kuandaa taarifa ya Mkoa kabla ya tarehe 1 Mei, 2022 alisema Mheshimiwa Hapi.

Mkuu wa Mkoa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa zoezi hilo kila baada ya wiki mbili kuanzia sasa.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa zoezi la uwekaji wa anuani za makazi ni muhimu sana kwa ajili ya utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi ambayo inategemewa kufanyika mwezi Agosti, 2022 hapa nchini.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali, vibao vya mtaa, vijiji na makazi binafsi serikali haitavitengeneza na badala yake wananchi watatengeneza vibao hivyo wao wenyewe.

Amewataka Wakuu wa Wilaya na Halmashauri kufanya mikutano ya kuwaelimisha wananchi kuhusiana na umuhimu wa zoezi hilo na namna wanavyoweza kushiriki.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa katika utekelezaji wa suala hilo, Wakala wa Barabara (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) wanatakiwa kuweka vibao vya mitaa inayogusana au inayochepuka kutoka barabarani katika barabara zote zinazojengwa sasa hivi au zitakazojengwa kuanzia sasa.

Mheshimiwa Hapi amezitaka Wilaya kuunda kamati maalum za utekelezaji wa zoezi hilo kuanzia ngazi za wilaya hadi katika vijiji na mitaa ili kufanikisha zoezi hilo.

Aidha amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa kila mtaa, Kijiji, maeneo ya biashara na makazi ya watu yanakuwa na vibao vya kuyatambulisha vinavyosomeka na kuonekana kiurahisi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa katika kutekeleza zoezi hilo serikali italeta fedha zenye maelekezo kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo, “hazitatumika kama fedha za OC, hizi zitakuwa na maelekezo maalum” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuwa Halmashauri zitoe msaada katika zoezi hili kwani zoezi linatakiwa kufanywa na watumishi wa umma na sio watu wa nje ya serikali” alisema Mheshimiwa Hapi. 

Awali, akisoma taarifa kuhusiana na miongozo ya serikali kuhusu anuani za makazi, Kaimu Afisa TEHAMA wa Mkoa Bwana Amon Stephano Mwasambungu ameeleza kuwa katika kutekeleza zoezi hilo  mfumo utakaotumika unasomana na GPS.

“Kwa hivyo baada ya kazi uthamini utafanyika katika ngazi mbalimbali hivyo zoezi linatakiwa kufanywa kwa umakini, uadilifu na ukweli katika ngazi zote” alisema Bwana Mwasambungu.  

Bwana Mwasambungu amezitaka Halmashauri kuwashirikisha Maafisa TEHAMA wa Halmashauri katika Kamati za kutekeleza jukumu hilo ili kufanikisha zoezi hilo kwa ufanisi zaidi.

Aidha, Bwana Mwasambungu amezitaka Halmashauri kutumia miongozo iliyotolewa na Serikali kuhusiana na anuani za makazi na ili kufanikisha zoezi hilo.

Zoezi la uwekaji wa anuani za makazi kitaifa lilianza mwaka 2017 katika baadhi ya mikoa hata hivyo kwa mwaka huu zoezi hilo litafanyika nchi nzima kuanzia tarehe 18 Februari 2022 hadi tarehe 01 Mei, 2022.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.