• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara Yazindua unyunyuziaji magari dawa

Posted on: April 17th, 2020

16 Aprili 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima leo amezindua zoezi la kunyunyuzia dawa ya kudhibiti Corona kwenye magari ya abiria katika setendi kuu ya mabasi ya Bweri iliyopo Musoma Mjini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo Mheshimiwa Malima amewataka wamiliki wote wa magari ya abiria kuhakikisha kuwa magari yote yananyunyuziwa dawa kabla ya kuondoka stendi ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wa magari hayo.

“Sisi kama serikali tuhakahikisha kila mmiliki na dereva wa magari anafuata utaratibu tuliojiwekea katika Mkoa wa Mara ili kuendelea kuwakinga watu wanaotumia magari haya” alisema Malima.

Aidha aliwahimiza wananchi wote kufuatilia maelekezo yote ya wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kunawa mikono, kuchukua tahadhari mbalimbali za kujikinga.

“Suala la kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka ni muhimu sana wakati huu na japokuwa linaonekana ni jambo rahisi likifanyiwa mzaha litawaathiri watu wengi zaidi.”

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa akiwa stendi ya Bweri alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu shida ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.

Akijibu malalamiko hayo, Mheshimiwa Malima amewataka Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) kuhakikisha maji yanapatikana kwa urahisi katika stendi hiyo ili kuwanusuru wananchi na wasafiri wanaotumia stendi hiyo kujikinga na corona na magonjwa mengine ya mlipuko.

Mkuu wa Mkoa katika uzinduzi huo aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, viongozi wa wilaya ya Musoma Mjini na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.  

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga alisema zoezi hilo litafanywa katika stendi zote za Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 16 Aprili 2020.

Aidha ameeleza kuwa utaratibu unataka magari kunyunyuziwa dawa nusu saa kabla ya kuanza kupakia abiria katika magari hayo.

“Hatua hii ni muhimu kwa ajili ya kuwalinda abiria na wafanyakazi wa magari haya ambao wanakutana na watu wengi waliotoka sehemu mbalimbali ili waweze kujilinda na corona” alisema Dkt. Tinuga

 Katika utaratibu huu wa kupuliza magari dawa, wamiliki wa magari watatozwa shilingi 5000 kwa mabasi makubwa, 3000 kwa basi ndogo (coaster) na shilingi 2000 kwa mabasi madogo madogo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.