• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yawahakikishia wananchi usalama wakati wa sikukuu

Posted on: December 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amezungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake na amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Mara usalama katika kipindi chote cha sikukuu za Noeli na Mwaka Mpya.  

“Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara imejipanga vizuri kuhakikisha kuwa Mkoa wetu unakuwa eneo salama wakati wote wa sikukuu hizi za mwisho wa mwaka” amesema Mhe. Mtambi,

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kutii sheria bila shuruti na kujiepusha na vitendo vya kiuhalifu na ametoa onyo kwa wanaopanga kufanya uhalifu wakati huu wa sikukuu kuacha kwani vyombo vya usalama vimejipanga kukabiliana na vitendo vya kihalifu.

Mhe. Mtambi amelitaka Jeshi la Polisi kuongeza doria katika maeneo yote wanayoishi wananchi na kuchukua hatua stahiki za kuzuia ajali barabarani kwa kuwadhibiti madereva wanaoendesha vyombo vya moto kwa uzembe na kuhatarisha maisha ya watu na mali zao.

“Ninawataka Askari wa Usalama barabarani kuanzia leo kuwa wakali kweli kweli na kuwachukulia hatua  za kisheria madereva wazembe barabarani,….hatuko tayari kuona wananchi wakipata madhira kipindi hiki cha sikuukuu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kutokuendesha vyombo vya moto wanapokuwa wamekunywa vileo na kuwataka kuchukua tahadhari za usalama ili kulinda usalama wao na familia zao wakati huu wa sikukuu.

Mhe. Mtambi amewataka wazazi na walezi kuendelea kusimamia maadili ya watoto wadogo kwa kuwazuia kwenda kwenye kumbi za starehe bila ya kuwa na uangalizi wa kutosha na hususan nyakati za usiku.

Kanali Mtambi amewakumbusha wazazi na walezi wakati wanasherekea sikukuu kukumbuka kutenga fedha za ada na mahitaji muhimu ya shule kwa ajili ya watoto ili kuwawezesha watoto kwenda shule shule zitakapofungua tena.

Mhe. Mtambi ametumia pia fursa hiyo kuwatakia wananchi wote wa Mkoa wa Mara heri ya sikukuu ya Noeli na Mwaka Mpya, 2025.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.