• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yatoa Mafunzo ya kudhibiti Corona kwa wafanyakazi

Posted on: May 4th, 2020

Mkoa wa Mara leo tarehe 4 Mei 2020 umetoa mafunzo ya namna ya kujikinga maambukizi ya ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (COVID 19) kwa wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa wafanyakazi wa ofisi hii ili waweze kutimiza wajibu wao wakiwa salama.

“Ninashukuru Katibu Tawala umeamua tuwe na haya mafunzo hapa, maana ugonjwa ukiingia hapa ofisini unaweza kuenea ndani ya muda mfupi sana na watu wengi kama hawatachukua tahadhari wataambukizwa” alisema Mheshimiwa Malima.  

Ameeleza kuwa kwa sasa tunapambana na kirusi ambacho hakijulikani vizuri hata kwa wataalamu wa afya na bado hamna dawa wala tiba ya ugonjwa unaosababishwa na kirusi hicho.

“Muhimu kwetu kwa sasa ni kupokea ushauri na maelekezo yote ya wataalamu wa afya lakini pia kuangalia njia za asili ambazo zimekuwa zikitumika katika kupambana na magonjwa mbalimbali katika jamii zetu” alisema Malima.

Ameeleza kuwa imani za watu pia kwa wakati huu ni muhimu sana, lakini imani isishindane na utaalamu wa kisayansi bali imani iendane na ushauri wa kitaalamu na maagizo ya serikali.  

Aidha Mheshimiwa Malima amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha wataalamu wa afya wanatoa elimu kwa watu wanaotengeneza barakoa ili waweze kutengeneza zinazokidhi vigezo vya kuwakinga watu na maambukizi.

Amewataka wafanyakazi na hususani ambao ni wataalamu wa afya kusaidia katika kuwapunguzia hofu walionayo wananchi wengi kwa sababu ya kutokuelewa na uvumi unaoenezwa kupitia mitandao ya kijamii.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wafanyakazi ili waweze kujikinga na kuwakinga wateja wao wanaowapa huduma.

“Ninachowaomba ni kuyapa umuhimu mkubwa mafunzo haya muda wote tutakapoendelea kuwa na Corona ili tuweze kujikinga na maambukizi haya na ninawataka wafanyakazi wote kuchukulia suala la kujikinga na maambukizi ya Corona kwa uzito mkubwa” alisema Bibi Mthapula.

Ameeleza kuwa leo tumepata elimu ya namna bora ya kuishi na Corona katika mazingira yetu na hususani ofisini ambako ndio tunakaa masaa mengi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Florian Tinuga ameshukuru kwa Katibu Tawala kuona uhumihimu wa kutoa mafunzo hayo kwa wafanyakazi ili waweze kujikinga na corona.

“Mafunzo haya yatatusaidia sisi wafanyakazi kwani yatatuelekeza tunawezeje kuishi na Corona huku tukifanya kazi vizuri” alisema Dkt. Tinuga.

Katika mafunzo hayo wafanyakazi pia wamepitishwa katika miongozo ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto na mwongozo wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa (TAMISEMI) juu ya namna ya kuzuia maambukizi ya Corona sehemu za kazi.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.