• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara Yatoa Ekari 124 kwa ajili ya kuimalisha usalama katika Ziwa Victoria

Posted on: March 5th, 2020

Mkoa wa Mara umetoa eneo la ekari 124 katika kijiji cha Nyabange, Wilaya ya Butiama katika fukwe za Ziwa Victoria kwa ajili ya upanuzi wa shughuli za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha Wanamaji.

Akizungumza katika ziara yake ya kukagua eneo hilo,  Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Jenerali Venance Mabeyo ameushukuru Mkoa wa Mara na mmiliki wa awali wa eneo hilo kwa kukubali kutoa eneo hilo kwa ajili ya ulinzi wa nchi.

“Eneo hili ni zuri na kubwa na linakidhi mahitaji ya jeshi kwa sasa, tunashukuru sana” alisema Jenerali Mabeyo.

Akizungumza wakati wa kuonyesha mipaka ya eneo hilo, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema amefurahi uamuzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania kuamua kupanua shughuli zake katika Ziwa Victoria na kuweka kikosi kikubwa katika Mkoa wa Mara.

Mhehsimiwa Malima alisema kuwa awali Mara ilikuwa na kikosi kiteule cha wanamaji ambacho kutokana na ufinyu wa eneo na udogo wake hakikuweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Ameeleza pia kutokana na juhudi za pamoja wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama Mkoa wa Mara, Mkoa umefanikiwa kudhibiti uvuvi haramu, magendo ya samaki na kuongeza mapato yatokanayo na Ziwa Victoria. “Kwa sasa hata upatikanaji wa samaki katika Ziwa Victoria hususan kwa Mkoa wa Mara umeboreshwa sana” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima, Mkoa wa Mara ndio wenye eneo kubwa la Ziwa Victoria na raslimali nyingi za ziwa kwa sasa baada ya mgawanyo wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Wilaya ya Rorya ndio wilaya pekee hapa nchini ambayo eneo lake kubwa lipo mwambao mwa ziwa.

“Kujengwa kwa kikosi cha wanamaji hapa Nyabange kutaleta manufaa makubwa ya kiuchumi, kijamii na kiusalama kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla” Alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa upande wake mmiliki wa awali wa eneo hilo Mzee Samweli Wambura Kishamuri alisema awali yeye alikuwa na eneo la ekari 240 na kati ya hilo ekari 124 ametoa kwa serikali na ekari 116 amebaki nazo mpaka sasa.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.