• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

MARA YAPONGEZWA KUPUNGUZA MATUKIO YA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: December 10th, 2024

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima tarehe 09 Desemba, 2024 amekuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia na kuupongeza mkoa wa Mara kwa kufanikiwa kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia.

Akizungumza katika maadhimisho hayo ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Ingwe, Wilaya ya Tarime, Mhe. Gwajima amesema Mkoa wa Mara siyo kinara tena wa vitendo vya ukatili wa kijinsia hapa nchini.  

“Tuiambie dunia ijue kuwa Mara imefanikiwa kushusha takwimu za ukatili wa kijinsia; na kama inawezekana Mara na Mikoa mingine inawezekana” amesema Dkt. Gwajima.

Mhe. Gwajima amesema kati ya Mikoa inayoongoza kwa matukio ya ukatili nchini ni Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara ambayo ina asilimia 43 kila mmoja huku Mkoa wa Mara ukishika nafasi ya tatu ukiwa na asilimia 28.  

Mheshimiwa Gwajima ameitaja mikoa mingine yenye ukatili wa kijinsia ni Mkoa wa Singida asilimia 20, Mkoa wa Tanga asilimia 19 na Mkoa wa Dodoma asilimia 18.

Dkt. Gwagima ameutaka Mkoa wa Mara kupambana na tatizo la ukatili wa kijinsia kwa kupeleka elimu zaidi kwa makundi mbalimbali ya wananchi ili kuwajengea uelewa kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia.  

Mhe. Gwajima amewapongeza wadaua wote likiwemo Jeshi la Polisi Tanzania, taasisi za umma na binafsi ambazo zimeungana kwa pamoja kusaidia kupunguza matukio kwa kutoa elimu na kuchukua hatua za kisheria pale inapohitajika.

Akizungumza wakati akimkaribisha Mhe. Gwajima, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya amesema Desemba 09 ya kila mwaka ni siku ya uhuru wa Tanzania Bara na sikukuu hii kwa Mkoa wa Mara inatumika kupinga ukatili wa kijinsia.

Bwana Kusaya amesema haya ni mapambano ya watu wote wananchi na viongozi na kwa Mkoa wa Mara shabaha yetu ni moja kumlinda mtoto na watu wenye mahitaji maalum.

“Kumlinda mtoto ni kumuunga mkono Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amenuia kumlinda mtoto wa Tanzania kwa gharama yoyote ile” amesema Bwana Kusaya.

Akizungumza katika hitimisho hilo la siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara Bwana Apolinary Lyambiko amesema kuwa mgodi huo unasaidia juhudi za kupinga ukatili wa kinjisia hapa nchini.

“Tumepokea tuzo saba katika kusimamia dhamira ya uwajibikaji katika jamii ikiwamo Kupinga Ukatili wa Kijinsia nchini Tanzania” amesema Bwana Lyambiko.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/ Rorya, Mark Nyera amemthibitishia Waziri Gwajima kuwa kampeni ya Kupinga ukatili wa Kinjisia, siku hizi 16 zimetumika vizuri kupaza sauti juu ya suala hilo.

Afande Nyera amesema makosa ya ukatili wa kinjisia kwa sasa yanapungua kutoka mwaka mmoja kwenda mwingine mathalani kutoka mwaka 2023 kwenda 2024 yakiwa chini ya matukio 2000.

Kamanda Nyera akisema kuwa siku hizo 16 zinahitimishwa siyo kwamba Jeshi la Polisi Tanzania linaweka silaha chini bali linaongeza nguvu katika mapambano hayo kwa kasi zaidi.

Wakati huo huo, Mhe. Dkt. Gwajima amekabidhi majiko ya gesi 222 kwa wananchi wa vijiji vinavyouzunguka mgodi wa Barrick North Mara yaliyotolewa na mgodi huo kwa lengo la kuwaepushia wananchi adha ya matumizi ya nishati ya kupikia isiyo salama.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na viongozi wa Serikali na taasisi za binafsi, watendaji wa Serikali na wananchi wa Wilaya ya Tarime.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.