• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yapokea walimu 50 kutoka Zanzibar

Posted on: September 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewapokea walimu zaidi ya 50 kutoka Chama cha Walimu Zanzibar walio katika ziara ya mafunzo na utalii katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza na walimu hao, Mheshimiwa Mzee amewapongeza walimu hao kwa kufanya utalii wa ndani na kuchagua kuutembelea Mkoa wa Mara wenye vivutio vingi vya utalii na kihistoria ya Taifa letu. 

“Mara ni sehemu ambayo ina vivutio vingi vya asili ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuongeza kuwa Mara ndio chimbuko la Tanzania” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara amefurahi sana kuona walimu hao wamekuja kufanya utalii na kujifunza katika Mkoa wa Mara na kuwataka warudi Mara watakapojisikia uchovu na msongo wa mawazo.  

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Mara ambaye ni mwenyeji wa walimu hao Bibi Suzan Shesha amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuweza kuonana na walimu hao pamoja na ratiba za shughuli zake kuwa nyingi.

“Sisi pamoja na wageni wetu tunashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuweza kukutana na walimu hawa, na tunakuahidi tutawatembeza maeneo yote watakayotaka kwenda na kuwapa ushirikiano wakati wote wakiwa katika Mkoa wa Mara” alisema Bibi Shesha.  

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) Bwana Musa Abdi Hamis ameeleza kuwa ziara yao pamoja na kujifunza kutoka katika shule mbalimbali za Mkoa wa Mara, watatembelea vivutio vya utalii na nyumbani kwa Baba wa Taifa ili kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhamasisha utalii kupitia filamu ya Royal Tour.

Bwana Hamis ameeleza kuwa katika ziara hiyo, watatembelea shule mbalimbali za msingi, shule za sekondari zinazofanya vizuri sana na zile ambazo hazifanyi vizuri katika mitihani ya Taifa ili kuweza kujifunza.

Aidha, walimu hao wanatarajia kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, maonyesho ya Mara International Expo yanayoendelea katika viwanja vya Mukendo, Manispaa ya Musoma, mpaka wa Tanzania na Kenya uliopo eneo la Sirari wilayani Tarime, Shule ya Msingi Mkendo aliyosoma Baba wa Taifa na nyumbani kwa Baba wa Taifa.

Walimu hao pia walitoa zawadi za viungo vya Zanzibar mbalimbali kwa Mkuu wa Mkoa na Chama cha Walimu Mkoa wa Mara.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.