• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yapokea miradi ya zaidi ya milioni 200

Posted on: January 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo amepokea nyumba ya walimu, mradi wa maji na ufadhili wa wanafunzi wenye jumla ya thamani ya shilingi 222,500,000 kutoka Shirika la Zawadi Project.

Akizungumza katika hafla ya kupokea msaada huo, Mheshimiwa Mzee amelipongeza shirika hilo kwa msaada huo ambao unaisaidia jamii katika shule mbalimbali za  Serikali katika kata saba za Tarafa ya Chamriho, Wilaya ya Bunda.

Miradi iliyopokelewa ni nyumba ya walimu yenye uwezo wa kuchukua familia sita yenye thamani ya shilingi 120,500,000/=, mradi wa kisima, matenki na mtandao wa maji wenye thamani ya shilingi 49,000,000/= na ufadhili wa wanafunzi 256 wa shule za msingi na sekondari wenye thamani ya shilingi 53,000,000/=

Akiwa katika eneo hilo, Mheshimiwa Mzee amezindua mradi wa maji katika Shule ya Msingi Kambarage na nyumba ya walimu katika Shule ya Msingi Sarawe zilizojengwa kwa nguvu ya wananchi na ufadhili wa shirika la Zawadi Project.  

Mheshimiwa Mzee amemtaka Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage kubuni namna ya kukifanya mradi wa maji waliopewa na Shirika la Zawadi kuwa endelevu na kuweza kuleta manufaa yaliyotarajiwa.

Awali, Mratibu Mkazi wa Shirika la Zawadi Project Bwana Nelson Mafie ameeleza kuwa Shirika hilo linafanya miradi yenye lengo la kutoa ufadhili kwa wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu, kuboresha mazingira ya shule na kutoa mafunzo ya walimu kazini.

Kwa mujibu wa Bwana Mafie, miradi iliyopokelewa leo ni mwendelezo wa miradi mbalimbali ambayo shirika hilo limekuwa likiitekeleza katika kata mbalimbali za Tarafa ya Chamriho, Wilaya ya Bunda.

Bwana Mafie ameeleza kuwa ufadhili wa wanafunzi ni kuanzia shule ya msingi hadi vyuo vikuu kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao.

Kwa mujibu wa Bwana Mafie ameeleza kuwa kwa sasa shirika linawafadhili jumla ya wanafunzi 256 ambapo kati yao wanafunzi 141 wapo shule za msingi, 115 wapo shule za sekondari 14 wapo Kidato cha Tano na Sita, 12 wapo katika mafunzi ya ufundi, 4 wapo vyuo vya kati na 7 wapo katika vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini.

 Bwana Mafie ameeleza kuwa shirika hilo lenye makao yake makuu katika Mkoa wa Arusha, Katika Mkoa wa Mara Shirika hilo linafanya shughuli zake katika Wilaya ya Bunda Tarafa moja ya Chamriho.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.