• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yaomba JKT kuongeza Uwekezaji katika Shamba Darasa la Mkoa

Posted on: December 17th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameliomba Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuwekeza zaidi katika Shamba Darasa la Mkoa wa Mara maarufu kama viwanja vya Mama Maria Nyerere vilivyopo katika Kijiji cha Butiama, Wilaya ya Butiama.

Mheshimiwa Malima ametoa ombi hilo leo tarehe 16 Desemba 2020 ofisini kwake baada ya kumpokea Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Charles Mbuge ofisini kwake akiwa katika ziara ya kutembelea Mkoa wa Mara.

“Kwa Mkoa wa Mara tungefurahi sana kama jeshi letu lingewekeza zaidi katika eneo tulilowatengea katika viwanja vya Mama Maria Nyerere ili wananchi wa Mkoa wa Mara waweze kujifunza na kufaidika na utaalamu wa kilimo uliopo JKT” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima amesema kuwa Mkoa uliamua kuanzisha shamba hilo ili kuweza kuwafikia wakulima wake kiurahisi zaidi katika kuwapa elimu, teknolojia na mifano ya kilimo bora kutoka kwa wataalamu na wakulima waliofanikiwa.

“Bado tunaendelea kushiriki katika maonyesho yanayofanyika katika viwanja vya maonyesho ya kilimo kwa Kanda ya Ziwa Mashariki kule Nyakabindi, Simiyu lakini shamba hili ni fursa kubwa zaidi kwa wakulima wetu maana hapa ni karibu na wanaweza kufika na kujifunza” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha amemshukuru Mkuu huyo kwa kazi kubwa ambayo JKT inaifanya katika kuhamasisha kilimo cha mazao ya kimkakati na hususan kahawa, pamba na mihogo katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake Meja Jenerali Mbugi ameeleza kuwa JKT kwa sasa imewekeza sana katika kilimo cha mazao mbalimbali hapa nchini na kwa sasa imeajiri watu sita ambao ni raia waliobobea katika utaalamu wa kilimo. 

“Tumepata mafanikio makubwa sana kutokana na uwekezaji katika kilimo na kuliwezesha jeshi kununua magari 27 na matrekta 10 kutokana na fedha za ndani” alisema Mkuu wa JKT.

Alisema kwa mwaka huu, JKT imewekeza zaidi katika kilimo katika mikoa na mazao mbalimbali ili kuweza kutoa mafunzo ya kilimo kwa wakulima na kuongeza mapato ya ndani ya jeshi hilo.

Ameahidi kuwa JKT itaongeza uwekezaji wake katika eneo walilopewa katika viwanja hivyo ili kutoa mafunzo kwa wakulima na kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mkoa wa Mara umeanzisha maonyesho ya kilimo katika viwanja vya Mama Maria Nyerere kuanzia mwaka huu ili kutoa mafunzo endelevu kwa wakulima kuhusu mazao ya kimkakati ya chakula na biashara ili kuongeza tija kwa wakulima wake.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.