• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yajipanga kutekeleza miradi

Posted on: November 5th, 2021

Mkoa wa Mara umeanza maandalizi ya kutelekeza miradi ya Elimu na Afya ambayo imeletwa kutokana na fedha za maambikizi ya Uviko 19 na sehemu ya fedha za zilizotokana na tozo.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha wasimamizi wa Mkoa wa miradi ya Elimu na Afya kilichofanyika leo tarehe 18 Oktoba 2021 katika Ukumbi wa Uwekezaji, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameeleza kuwa fedha za miradi zilizoletwa wakati huu ni nyingi.

“Haya ni mapinduzi makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wake Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ili kuimarisha huduma za jamii katika maeneo ya Elimu, Afya, Barabara na kadhalika” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ameeleza kuwa serikali imeleta shilingi 1,550,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya sita kutokana na fedha za tozo; shilingi 3,190,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya huduma za dharura; na shilingi 1,400,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 618 ya shule za sekondari kupitia Mpango wa Maendeleo ya Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa katika fedha zilizoletwa hamna bajeti ya usimamizi na ufuatiliaji wa mradi hii na hivyo hatarajii watendaji kutumia fedha hizo kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji.

Kikao cha Mkoa cha kujadili utekelezaji wa miradi hiyo kiliazimia kuanzisha mfumo wa kidigitali wa kufuatilia utekelezaji wa miradi yote inayotelezwa ndani ya Mkoa ili kuweza kupata taarifa za miradi hiyo kila siku.  

Amewaelekeza Wakurugenzi wa Hamashauri kuhakikisha kuwa madarasa yanayoenda kujengwa kwa kutumia fedha hizo ni mapya na sio kukamilisha maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

“Tunataka miradi hii ijitegemee na isichanganywe na maboma yaliyojengwa na wananchi au Halmashauri hapo awali” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuunda kamati za ujenzi ndani ya wiki hii na kuanza kutafuta sehemu ya kupata vifaa vya ujenzi wakati wakisubiri maelekezo kuhusu matumizi ya fedha hizo kutoka serikalini. 

Amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakrugenzi wa Halmashauri kuwatangazia vijana fursa zinazotokana na miradi hii katika maeneo yao ili waweze kuchangamkia fursa hizo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.