• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yajipanga kupokea wageni

Posted on: February 1st, 2022

Mkoa wa Mara umejipanga kuwapokea wageni mbalimbali watakaokuja kushiriki kilele cha maadhimisho ya miaka 45 ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ziara ya Mheshimiwa Rais kuanzia tarehe 4-7 Februari, 2022.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametoa kauli hizo leo tarehe 1 Februari, 2022 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Mkoa unatarajia kupokea wageni takriban 5,000 katika kipindi hiki na niwahakikishie watapata huduma za malazi, usafiri, mawasiliano na mahitaji mengine muhimu wakati wote wakiwa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewahakikishia watanzania kuwa tayari uongozi wa Mkoa wa Mara umefanya mazungumzo na wafanyabiashara mbalimbali wanaotoa huduma na kuwataka watoe huduma kwa weredi, usafi na viwango vinavyokubalika wakati huu.

“Tumeamua katika kipindi hiki chote baa, kumbi za starehe na sehemu za chakula zitanyakazi kwa masaa 24 ili kuwawezesha wageni kupata huduma kiurahisi zaidi wakati wote wanapohitaji” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka wafanyabiashara wa Mkoa wa Mara kutumia fursa hii kikamilifu ili kuweza kujitangaza na kujiimarisha katika biashara zao na hususan biashara za huduma mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, amewahakikishia wageni wote kuwa Mkoa wa Mara upo salama siku zote na wakati wote wa ziara ya Mshehimiwa Rais itafanyika kwa utulivu na amani.

Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuwasaidia wageni mbalimbali watakaohitaji kujua kuhusiana na maeneo muhimu na sehemu za kupata huduma mbalimbali.  

“Mimi ninajua kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara ni wakarimu na wanapenda sana wageni hivyo sina mashaka kwamba wageni watapokelewa vizuri katika ziara hiyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi amewahimiza wananchi wote kuishi kwa amani, upendo na utulivu wakati wote ambapo Mkoa una wageni ili wageni wakalitangaze vyema jina la Mkoa wa Mara huko waendako.   

 Wageni wanaotarajia kushiriki ziara hii ya Mheshimiwa Rais ni pamoja na Viongozi Wakuu wa Kitaifa, Viongozi wa Kitaifa waliostaafu, viongozi na makada wa Chama cha Mapinduzi, Wabunge, Viongozi mbalimbali wa Serikali, wafanyabiashara, wanachama wa CCM na wananchi wa kawaida.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.