• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yajipanga kunufaika na Serengeti

Posted on: July 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameeleza kuwa Mkoa wa Mara unajipanga kuanza kunufaika zaidi na uwepo wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti katika Mkoa wa Mara.

Hayo yameelezwa leo katika hafla ya makabidhiano ya ofisi kati ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Eng. Robert Gabriel Luhumbi na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi yaliyofanyika katika ukumbi wa uwekezaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Maafisa wa TANAPA (Mamlaka ya Hifadhi za Taifa) walikuja leo ofisini kwangu wameniambia kuwa Hifadhi yote ya Taifa ya Serengeti ipo katika Mkoa wa Mara, pale ambapo Hifadhi ya Serengeti inapoishia ndio mpaka wa Mkoa wa Mara na Mkoa wa Arusha, jambo ambalo limenishangaza sana” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa awali alidhania asilimia 70 ya ardhi ya Serengeti ndio ipo katika Mkoa wa Mara jambo ambalo ameelezwa na Mhifadhi Mkuu wa TANAPA Kanda ya Magharibi kuwa sio sahihi, eneo lote la hifadhi lipo katika Mkoa wa Mara.

Ameeleza kuwa watu wanaifungamanisha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Arusha kwa sababu ya miundombinu ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na Uwanja wa Ndege wa Arusha na miundombinu mingine ambapo watalii wengi wamekuwa wakiitumia kwa ajili ya kuja Serengeti na kufanya wanufaika wakuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuwa ni Arusha.

“Tunaenda kufanyakazi kubwa sana ya kuutangaza Mkoa wa Mara ndani na nje ya nchi ili wawekezaji waweze kuelewa mambo mazuri na fursa za uwekezaji zilizomo katika Mkoa wa Mara ili wananchi wa Mara waweze kuonja matunda ya fursa zilizopo katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa baada ya uwanja wa ndege wa Musoma unaoendelea kupanuliwa kukamilika, ndege kubwa za abiria zitarudi Musoma jambo ambalo litarahisisha watalii wengi kuingia Serengeti wakitokea Musoma kwa urahisi zaidi kuliko ilivyo sasa.

Ameeleza kuwa Mkoa wa Mara unautajiri mkubwa sana wa madini mbalimbali, Ziwa Victoria na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ni urithi wa dunia katika utalii.

“Tunataka uchumi na uwekezaji utakaofanyika Mkoa wa Mara ufanane na wingi wa utajiri wa asili uliopo, hili ndilo jambo mimi na wenzangu tunaenda kulifanyia kazi kwa haraka sana ili wananchi waweze kufaidi matunda ya utajiri uliopo katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa umejikita zaidi katika kuhamasisha ujenzi wa mahoteli ya kisasa katika Mji wa Bunda na Mugumu ambayo ni malango makuu ya kuingilia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Ametoa mfano wakati wa Serengeti Marathon ambayo hufanyika mwezi Novemba ya kila mwaka, watu wengi wanaohudhuria wanakosa vyumba vya kulala na kulazimika kulala mbali na Mji wa Bunda hivyo ameeleza kuwa panahitajika uwekezaji mkubwa.

Mheshimiwa Hapi amewaomba wananchi na viongozi wa Mkoa wa Mara kutoa ushirikiano kwa viongozi wa Mkoa ili Mkoa uweze kupiga hatua katika maendeleo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Eng. Robert Gabriel Luhumbi amemkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mara kuendelea kazi mbalimbali ambazo yeye na watangulizi wake walikuwa wamezianza.

Mheshimiwa Hapi amehamishiwa Mara kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi ambaye amehamishiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko tarehe 11 Juni 2021. 

Makabidhiano hayo pia yalihudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Viongozi wa Wilaya, Halmashauri, viongozi wa dini, watendaji wa Sekretariati ya Mkoa wa Mara, wakuu wa taasisi za umma na waandishi wa habari.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.