• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yajipanga kuanza kulima Mkonge

Posted on: February 23rd, 2021

Mkoa wa Mara unampango wa kuanza kulima zao la mkonge kama zao kuu la biashara kwa wakazi wa Mkoa wa Mara katika msimu huu wa kilimo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 19 Februari 2021, Mkuu Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amesema kwa kuanzia Mkoa umeazimia kulima ekari 6,000 katika halmashauri za wilaya za Bunda, Butiama, Musoma, Rorya, na Serengeti. 

“ Kwa sasa tayari halmashauri hizi zimetenga maeneo ya ekari 10 kila mmoja kwa ajili ya kuanzisha vitalu vya miche ya mkonge na kisha kuwagawia wakulima watakaolima mkonge katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa ili kulima ekari hizi 6,000 Mkoa umeaagiza miche 10,400,000 kutoka Tanga.  

Aidha Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa Mkoa pia kwa kushirikiana na Pamba Mara Cooperative Limited unampango wa kuchukua mkopo wa shilingi bilioni 2.5 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa ajili ya kufadhili shughuli za uendelezaji wa zao la Mkonge katika Mkoa wa Mara.

“Fedha hizi pamoja na mambo mengine zitatumika kulima shamba, kununua matrakta matatu, kufanya utafiti wa udongo, kufadhili gharama za mafunzo ya maafisa ughani 40 ambayo yatatolewa na Chuo Kikuu cha Mwalimu J. K. Nyerere, Butiama” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha mheshimiwa Malima ameeleza kuwa katika malengo ya muda mrefu, Mkoa wa Mara unampango wa kulima ekari 30,000 za zao la mkonge katika halmashauri hizo sita.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri, waandishi wa habari na wadau wengine kuhamasisha kilimo cha zao la mkonge katika halmashauri zao ili kuweza kuinua hali ya uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Mara.

 Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima Mkonge sio zao geni katika Mkoa wa Mara liliwahi kulimwa miaka ya zamani katika baadhi ya maeneo hata hivyo baadaye liliachwa kutokana na kukosa usimamizi na soko la uhakika.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.