• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yadhamiria kuboresha barabara

Posted on: November 29th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka wakandarasi waliopewa zabuni za kujenga barabara mbalimbali katika Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao kikamilifu kwa mujibu wa mikataba yao.

Mheshimiwa Hapi ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Uwekezaji uliomo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Hatutakubali, hatutawavumilia wala hatutawafumbia macho wakandarasi wababaishaji ambao wanalipua kazi na kutokulipa wafanyakazi wao, wasiotekeleza kazi kwa haraka” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara walioko vijijini wanategemea sana barabara za TARURA na kutoa rai kuwa barabara zitakazofanyiwa kazi zilenge katika kuwasaidia wananchi kujenga uchumi wao na kuwaunganisha wananchi na huduma za kijamii.

Amezitaka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kutoa mafunzo kwa wakandarasi wa Mkoa wa Mara ili kuwajengea uwezo waweze kutekeleza miradi kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Mheshimiwa Hapi amezitaka taasisi hizo wakati wa kutoa zabuni kwa wakandarasi kutoa kipaumbele kwa wakandarasi ambao wanauwezo, wasio na ubabaishaji katika kutekeleza miradi kwa mujibu wa mikataba yao.

“Hatutawapa kazi wakandarasi wa Mkoa wa Mara kwa kwa sababu tu ni wenzetu, tunawafahamu” alisema Mheshimiwa Hapi na kuwataka wakandarasi watekeleze miradi kwa viwango vinavyokubalika bila ubabaishaji.

Aidha amewataka Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Mara kuaajiri watu kutoka katika maeneo wanapofanyia kazi hususan zile kazi ambazo hazihitaji ujuzi maalum ili kutoa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Mara

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya kusimamia miradi ya barabara inayotekelezwa katika maeneo yao na kuifuatilia kwa karibu kuweza kujiridhisha kuhusu hali halisi ya miradi hiyo.

Wakati huo huo, Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mara kimemchagua kwa kauli mmoja Mheshimiwa Jumanne Sagini, Mbunge wa Butiama, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Sagini ambaye ni Katibu Mkuu na Katibu Tawala Mstaafu amechaguliwa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kupendekeza jina lake na wajumbe wa kikao hicho kuridhia kwa kauli mmoja.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Meya na wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi wa serikali za mitaa, Kamati ya Usalama ya Mkoa, wasimamizi wa masuala ya usafiri na Sekretarieti ya Mkoa na wadau wa usafiri katika Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.