• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yaboresha Mazingira ya Uwekezaji

Posted on: February 28th, 2020

Mkoa wa Mara umedhamiria kuwa kinara wa biashara na uwekezaji kwa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji mkoani humo. Hayo yameelezwa katika Mkutano wa Mashauriano kati ya serikali,  wafanyabiashara na wawekezaji uliofanyika tarehe 24 Februari 2020 katika ukumbi wa Mwembeni, Manispaa ya Musoma.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkuatano huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Malima amesema Mkoa wa Mara unajipanga kuweza kuongeza uzalishaji na tija ya shughuli mbalimbali zinazofanyika katika mkoa huu ikiwa ni pamoja na kilimo cha Kahawa na Pamba.

“Kwa muda mrefu Mara ni Mkoa ambao fursa zake na raslimali zake zilikuwa zimejificha na kunufaisha mikoa mingine. Kama Mkoa tumeamua kutangaza fursa na rasilimali mbalimbali zilizomo ili kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara zaidi.”

Akitoa mfano wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, mazao yatokanayo na Ziwa Victoria na madini yaliyopo mkoani humo, ambavyo awali vilikuwa vinainufaisha mikoa na nchi jirani lakini vipo katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mara, Bwana Boniface Ndengo amesema taasisi yao inalengo la kuufanya Mkoa wa Mara kuwa lango kuu la biashara kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa. “Tumechukua jitihada za maksudi kuhakikisha tunawakuza wafanyabiashara na wawekezaji wa Mkoa wa Mara ili kuuwezesha Mkoa wetu uweze kukua kiuchumi”  

Mkutano huo ulihudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mheshimiwa Angela Kairuki, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mheshimiwa Mhandisi Stella Manyanya. Aidha ulihudhuriwa pia na maafisa mbalimbali wa serikali ikiwemo wawakilishi wa Makatibu wakuu wa wizara, wakuu wa taasisi, wawakilishi wa wakuu wa taasisi na maafisa waandamizi wa serikali.

 Mkutano huo pia ulihudhuriwa na viongozi wote wa Mkoa wa Mara, wawakilishi kutoka katika vyama mbalimbali vya wafanyabiashara, wawekezaji pamoja na wakuu wa taasisi zote zilizomo katika Mkoa wa Mara. Katika Mkoa wa Mara mkutano huu umefadhiliwa na Kampuni ya Barrick kupitia mgodi wake wa North Mara, Benki ya NMB na Benki ya NBC.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • RC atoa siku 14 wanafunzi wote Sekondari ya J. K. Nyerere wapate chakula shuleni

    July 28, 2025
  • Kusaya apokea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama

    July 25, 2025
  • Mtambi ataka matumizi ya GOTHOMIS kwa asilimia 100 Mara

    July 25, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.