• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yaanza Kuchukua Hatua

Posted on: February 17th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameanza kuchukua hatua mbalimbali katika utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoyatoa katika ziara yake mkoani Mara tarehe 4-7 Februari, 2022.

Akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya miradi kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji Mheshimiwa Hapi ameagiza mamlaka zinazohusika kuwasimamisha kazi watumishi saba kutokana na makosa mbalimbali katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Mara. 

“Hawa wamekuwa wanatuhumiwa kuwa na matatizo mbalimbali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mara, sasa wasimamishwe ili kupisha uchunguzi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Watendaji aliyoelekezwa wasimamishwe ni Bi. Mariam Chacha, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Halmashauri ya Wilaya ya Tarime; Mhandisi Maige James Gibai, Mkuu wa Idara ya Uhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma; Bi. Maria Nyandoro Chokongoye Mhasibu wa Mapato wa Hamashauri ya Wilaya ya Musoma na Bwana Joseph Orest Luhwa maarufu kama Msuya Afisa katika Idara ya Uvuvi katika Manispaa ya Musoma.

Watendaji wengine ni Bwana Leonard Lukawe Mkau Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Bwana Buzana M. Kazare, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Bwana Nzaya Muhoja, Afisa Manunuzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWASA)

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kufuatilia utendaji wa Waganga Wakuu wa Halmashauri za Wilaya za Tarime, Bunda na Musoma, Mweka Hazina wa Manispaa ya Musoma na Afisa Elimu wa Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Aidha katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa pia amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya za Musoma, Bunda na Tarime kujieleza kwa maandishi kwa nini Halmashauri zao hazikuomba fedha za miradi ya maendeleo iliyotengwa katika bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa mujibu wa utaratibu wa fedha za miradi ya maendeleo.

“Tangu tumeanza kutekeleza bajeti ya mwaka huu, huu ni mwezi wa nane sasa tumeanza lakini hawa hawajaomba fedha hizo na miradi hii haijaanza kutekelezwa, wakati wengine wameshaomba na tayari fedha hizo wameshapata na zimeanza kutekeleza miradi iliyopangwa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa fedha hizo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya miradi ya elimu, afya, nyumba za watumishi na ofisi za Halmashauri.

Fedha ambazo hazijaombwa mpaka sasa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ni Tshs. 2,875,000,000/=, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Tshs.2,362,500,000/=, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Tshs. 1,862,5000,000/=.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara kufanya uchunguzi katika mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Watu wenye Ulemavu na Vijana ili kubaini uwepo wa mikopo hewa na kuwasilisha taarifa kwa Mkoa wa Mkoa ndani ya wiki mbili. 

Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri na Wilaya ya Bunda kwa kushirikiana na Kamati ya Usalama ya Wilaya kufanya uchambuzi wa maafisa wanaokaimu ambao baadhi yao wanatuhumiwa kuhujumu uchunguzi unaoendelea kufanyika.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa wiki mbili kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha fedha zote za mapato ya ndani ambazo hazijaingizwa benki ziwe zimeingizwa na Wakurugenzi wa Halmashauri wawasilishe wawasilishe majina ya wahusika wote waliokula fedha mbichi na hatua zilizochukuliwa.

“Kwa sasa hivi halmashauri zote zinafedha ambazo zimekusanywa kama mapato ya ndani na hazijaingizwa benki kiasi cha bilioni 1.795 sasa ninataka kupata taarifa ya pesa hizi mbichi zipo kwenye akounti za halmashauri au ni nani aliyekula tushughulike nae” alisema Mheshimiwa Hapi.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Meya wa Manispaa ya Musoma, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wakuui wa Taasisi, Wakuu wa Polisi wa Wilaya zote za Kipolisi katika Mkoa wa Mara, Makamanda wa TAKUKURU wa Wilaya na Maktibu Tarafa wote wa Mkoa wa Mara.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.