• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yaaimarisha udhibiti wa Uvuvi Haramu

Posted on: June 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kwa kununua boti ya doria kwa ajili ya udhibiti wa uvuvi haramu katika Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Malima ametoa pongezi hizo tarehe 4 Juni 2020 wakati akizindua rasmi boti ya kisasa iliyonunuliwa na Manispaa ya Musoma kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu.

“Mimi ninawapongeza sana Manispaa ya Musoma kwa kuwa Halmashauri ya kwanza katika Mkoa wa Mara kwa kununua boti itakayoongeza nguvu katika mapambano dhidi ya uvuvi haramu katika Ziwa Victoria” alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa jitihada mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na Mkoa wa Mara katika kulinda raslimali za ziwa ikiwemo kudhibiti uvuvi haramu na ununuzi wa boti hiyo ya kisasa utaimarisha zaidi jitihada hizo na matokeo ni kuongezeka kwa samami na mapato yatokanayo na uvuvi.

Mheshimiwa Malima ameitaka Halmashauri hiyo kuitunza boti hiyo ili itumike muda mrefu kwa manufaa ya wananchi wa Manispaa ya Musoma.

Aidha amempongeza sana Mkuu wa Wilaya ya Musoma kwa kuwa mstari wa mbele katika juhudi za kudhibiti uvuvi haramu katika Mkoa wa Mara. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Vincent Naano Anney ameeleza kuwa halmashauri zote mbili za wilaya hiyo zimeongeza sana makusanyo yanayotokana na uvuvi tangia serikali ya awamu ya tano iingie madarakani na hivyo ununuzi wa boti hii unalenga kuimarisha jitihada hizo.

Ameeleza kuwa halmashauri za Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma zinapata jumla ya makusanyo ya shilingi 1.2 bilioni kwa mwaka.

“Kabla ya kuimarisha udhibiti, halmashauri zote mbili zilikuwa zinapata kiasi cha shilingi 160,000 tu kwa mwaka na sasa makusanyo yamepanda maradufu” alisema Dkt. Naano.

Boti hiyo ya kisasa inauwezo wa kuchukua abiria nane na inauwezo wa kukimbia zaidi ya boti za awali zilizokuwa zinatumika katika kudhibiti uvuvi haramu na imenunuliwa kwa gharama ya shilingi milioni 39 ikiwa na vifaa vya usalama.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.