• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara yaadhimisha miaka 60 ya Muungano kwa kupanda miti

Posted on: April 23rd, 2024

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Moses Kaegele leo ameongoza zoezi la kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Butiama ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania na kuwataka wananchi kuhifadhi mazingira kwa kupanda miti.

Mhe. Kaegele ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama ametoa rai hiyo wakati wa zoezi la upandaji miti 1000 katika eneo hilo na kuwataka wanafunzi kuwaelimisha wazazi, walezi na jamii kwa ujumla umuhimu wa kupanda miti kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.

“Watu wakipanda miti kwa wingi, watatunza mazingira na kupata faida mbalimbali za kijamii na za kiuchumi ambazo hazitapatikana kama nchi yetu haitakuwa na miti ya kutosha ili kuhifadhi mazingira yetu” amesema Mhe. Kaegele.

Mhe. Kaegele amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wazuri katika kupanda miti na kutunza miti iliyopandwa na kuwa mfano bora katika utunzaji wa mazingira.

Mwakilishi huyo wa Mkuu wa Mkoa ametumia nafasi hiyo kuwaonya watu wote wanaojihusisha na biashara ya mkaa na kuni bila ya kuwa na vibali na leseni zinazohitajika kuendesha biashara hiyo na kuahidi kuwa serikali itawachukulia hatua kali watakaobainika kukiuka sheria, kanuni na taratibu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bwana Emanuel Makoye ameeleza kuwa utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ni muhimu sana na kama hakuna uhifadhi wa mazingira hakuna maisha.

“Tunapoyatunza mazingira tunajiepusha na athari nyingi kutokea na tunatunza vyanzo vya maji na tunajilinda dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi” amesema Bwana Makoye.

Bwana Makoye ameeleza kuwa kwa kupanda miti jamii inapata manufaa makubwa ya kiuchumi na kijamii na kuwataka wanafunzi kuwa mabalozi wazuri katika utunzaji wa mazingira.

Bwana Makoye ameeleza kuwa katika maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania, jumla ya miti 1000 inategemewa kupandwa katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na misindano, mikongo, mikaratusi na misandawe.   

Kwa Mkoa wa Mara maadhimisho haya yamefanyika katika Halmashauri zote tisa kwa kufanya shughuli za usafi wa mazingira, kupanda miti, michezo na kuwasaidia wahanga wa mafuriko katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

 Maadhimisho ya miaka 60 kitaifa yanategemea kufanyika tarehe 26 Aprili, 2024 katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam yakiwa na kauli mbiu inayosema: Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa letu.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.