• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara Kuboreha Usafi wa Mazingira

Posted on: September 3rd, 2021

MARA KUBORESHA USAFI WA MAZINGIRA  

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi kesho tarehe 4 Septemba 2021 atazindua Kampeni ya Usafi wa Mazingira kwa Mkoa wa Mara kwa kufanya usafi katika Soko Kuu la Musoma lililopo katika Manispaa ya Musoma kuanzia saa moja  asubuhi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kampeni hii ni endelevu na inalengo la kuungarisha Mkoa wa Mara na itafanyika katika kila nyumba, mtaa, vijiji, kata, tarafa, halmashauri na wilaya zote za Mkoa wa Mara.

“Tumejipanga kuhakikisha Mkoa wetu unaondokana na magonjwa yanayotokana na uchafu ambayo yanawaathiri wananchi wetu kwa kusimamia usafi wa mazingira yanayotuzunguka” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa taifa linatumia fedha nyingi kukabiliana na changamoto za kiafya zinazotokana na uchafu na kuwataka viongozi na wataalamu wanaohusika kusimamia usafi katika maeneo yao.

“Tunampango wa kuanzisha mashindano ya usafi hususan katika ngazi ya wilaya na halmashauri zote za Mkoa wa Mara ili kupata halmashauri au wilaya safi na chafu zaidi na baadaye tutakuja kupata nyumba safi zaidi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewaagiza Maafisa Afya wote wa Mkoa wa Mara kusimamia usafi kwenye mazingira yao na kusimamia sheria, taratibu na miungozo ya usafi na utunzaji wa mazingira.  

Uzinduzi wa Kampeni ya afya katika Mkoa wa Mara utahudhuriwa na watumishi wote wa umma, vyombo vya ulinzi na usalama, wananchi na wataalamu wa afya na utafanyika katika maeneo mbalimbali ya wilaya zote sita za Mkoa wa Mara.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma inaonyesha kuwa Katika Manispaa ya Musoma usafi utafanyika katika kata zote za manispaa hiyo kuanzia saa moja asubuhi.

Katika Kata ya Kitaji usafi utafanyika katika eneo la Soko Kuu mjini, Stendi ya zamani, barabara ya Nyerere na Bustani ya Malkia; katika Kata ya Mushikamano usafi utafanyika katika Soko la Saanane, Barabara ya Samia S. H., Barabara ya Kwangwa na eneo la maduka saba; katika Kata ya Mukendo safi utafanyika katika barabara ya Mukendo, maeneo ya Kituo Kikuu cha Polisi, Shule ya Msingi John Bosco na eneo la TRA.

Katika Kata ya Mwigobero usafi utafanyika mwaloni, kivukoni na barabara ya Mwigobero; katika Kata ya Iringo usafi utafanyika katika Mtaro wa Kemondo, Barabara ya Mukendo na Muendo Kati; katika Kata ya Nyasho usafi utafanyika katika soko la Nyasho, Standi ya Nyasho na eneo la Mlango Mmoja.

Katika Kata ya Nyakato usafi utafanyika Musoma basi, barabara za makaburini, Nyerere na Baruti Sekondari, Shule ya Msingi Nyakato, eneo la SIDO na Maziwa; katika Kata ya Bweri usafi utafanyika katika maeneo ya Kariakoo, Stendi ya Bweri, Bweri Centre; na katika Kata ya Rwamlimi ni katika maeneo ya machinjioni na mwalo wa Narusulya.

Aidha katika kata ya Kamnyonge usafi utafanyika katika maeneo ya Majita Road, FFU na Uwanja wa Karume; katika kata ya Nyamatare usafi utafanyika katika soko la Nyamatare wakati katika Kata ya Makoko usafi utafanyika katika mwalo wa Makoko Ziwani.

Ili kufanikisha Kampeni ya Usafi itakayozinduliwa, wananchi wote mnaombwa kushiriki usafi maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na katika maeneo ya kuzunguka nyumba za kuishi.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.