• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Mara kuanzisha daftari la wahandisi katika miradi ya ujenzi

Posted on: July 12th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuanzisha daftari maalum la wataalamu wa Uhandisi litakalowekwa katika miradi yote ya ujenzi na ukarabati katika Halmashauri zao ili kurahisisha uwajibikaji wa wahandisi katika utekelezaji wa miradi.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Julai, 2022 kwa nyakati tofauti wakati akihudhuria vikao vya mabaraza ya madiwani katika Halmashauri za Wilaya ya Musoma na Manispaa ya Musoma.

“Ninataka kuwepo na madaftari maalum ambayo wahandisi watayatumia kutoa maelekezo kwa mafundi na wasimamizi wengine wa miradi na kutoa maoni yao ili kurahisisha uwajibikaji wa wahandisi katika miradi ya maendeleo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa amebaini katika baadhi ya miradi ya ujenzi wahandisi hawaitembelei mpaka viongozi wanapoenda kuitembelea na baada ya hapo hawarudi tena kurekebisha mapungufu waliyoelekezwa kuyarekebisha.

“Sasa tunataka mhandisi aidhinishe kila hatua ya mradi kwa maandishi na atoe maelekezo yake yote kuhusiana na mradi kwa maandishi ili kiongozi yoyote akifika katika mradi huo aweze kuyaona ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maendeleo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya na Madiwani kuhakikisha kuwa wahandisi wanasimamia miradi ya ujenzi kwa kukagua madaftari ya miradi na kuchukua hatua kwa wahandisi kwa kukwamisha miradi au hasara itakayotokana na utekelezaji mbovu wa mradi husika.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa anaamini madaftari hayo yakisimamiwa vizuri yataimarisha uwajibikaji wa wahandisi, kuboresha usimamizi wa miradi na kupunguza hoja za CAG na mbio za Mwenge wa Uhuru.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kuanzia sasa, kila atakapotembelea mradi atataka kuona madaftari hayo pamoja na maoni au maelekezo yaliyotolewa na wahandisi katika usimamizi wa miradi ya ujenzi na ukarabati katika Mkoa wa Mara.

Maagizo hayo yametolewa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kutembelea Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuhudhuria vikao vya mabaraza ya madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyoanza leo.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.