• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Malima: Uchunguzi Unaendelea

Posted on: April 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amezungumzia maendeleo ya uchunguzi uliokuwa unafanyika kuhusiana na watu waliohisiwa kukwama chini ya Mgodi wa North Mara walipoingia humo kwa nia ya kuiba.  

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 9 Aprili 2021 Mheshimiwa Malima amesema kuwa kwa sasa hamna watu waliokwama chini ya mgodi lakini uchunguzi unaonyesha kuwa kulikuwa na watu walioingia na kutoka chini ya mgodi huo.  

“Kwa sasa vyombo vya dola vinahitaji kuwahoji watuhumiwa watano ambao walikuwa wanajihusisha na kufadhili makundi ya vijana waliokuwa wanakwenda kuiba ndani ya Mgodi wa North Mara kwa mahojiano zaidi” alisema Mheshimiwa Malima.

Amewataja watuhumiwa kuwa ni Bwana Rafael Matiku Zakaria ambaye ni mfanyabiashara katika eneo la Bweri, Manispaa ya Musoma; Bwana Keraha Yohana Shona ambaye ni mfanyabiashara katika eneo la Nyamongo wilayani Tarime na Bwana Manase Kazota Philemon mkazi wa Buswelu mkoani Mwanza.

Watuhumiwa wengine ni wanaohitajika katika ukamilishaji wa uchunguzi huo ni Bwana Makenge Chacha Nyaisa mkazi wa Nyamwaga, Tarime na Bwana Nyagwisi Charles Marwa Mkazi wa Tarime.

“Watuhumiwa wote hawa wanatakiwa kujisalimisha katika ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara au Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Tarime/Rorya haraka iwezekanavyo kabla jeshi halijaanza kuwatafuta” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kwa pamoja wamekuwa wakifadhili baadhi ya vijana kuingia katika Mgodi wa North Mara unaomilikiwa kiubia kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya Barrick.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Malima ameongelea kuhusiana na maendeleo ya uchunguzi wa udanganyifu uliofanyika katika malipo ya fidia kwa wananchi wa vijiji viwili katika eneo la Nyamongo.

“Uchunguzi umefikia katika hatua nzuri na kwa sasa watuhumiwa 16 wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili” alisema Malima.

Ameeleza kuwa mpaka sasa uchunguzi umebaini katika ya fedha zote zaidi ya bilioni 30 zilizolipwa fidia, zaidi ya bilioni mbili zililipwa kwa watu waliotoa vielelezo visivyo sahihi na hivyo hawastahili malipo hayo.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.