• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Malima: Toeni Elimu ya Uchaguzi

Posted on: August 24th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa kutoa elimu zaidi kuhusiana na masuala muhimu ya uchaguzi kwa wasimamizi na wadau wa uchaguzi ili kuimarisha demokrasia hapa nchini.

Mheshimiwa Malima amesema hayo leo tarehe 24 Agosti 2020 ofisini kwake wakati alipowapokea maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Kanda ya Ziwa Mashariki ambao watasimamia uchaguzi katika Mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga.

“Wasimamizi wa uchaguzi kwa ngazi zote wanahitaji elimu ya sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kuimarisha demokrasia yetu hapa Tanzania”. Alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa elimu juu ya sheria hizi katika ngazi mbalimbali za usimamizi wa uchaguzi itaongeza uwajibikaji na kuimarisha picha ya demokrasia ya Tanzania kwa wadau wote ambao wangependa kuufuatilia.  

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kuna baadhi ya vyama vinajua kabisa havitashinda lakini vitajitahidi kuwekeza katika kuleta chokochoko ili kuvuruga uchaguzi na kuionyesha dunia kuwa uchaguzi wa Tanzania haukuwa wa haki.

Aidha Mheshimiwa Malima amemwagiza Mratibu wa Masuala ya Uchaguzi katika Mkoa wa Mara Bwana Dominick Rusasi kuandaa mafunzo ya sheria za vyama vya siasa na gharama za uchaguzi kwa Makatibu Tarafa na Watendaji wa Kata wa Mkoa wa Mara ili kuimarisha usimamizi wa uchaguzi.

Awali, maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyamavya siasa waliotoa pendekezo la kutoa mafunzo kuhusiana na sheria hizo kwa wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya majimbo na wasimamizi wa uchaguzi kwa ngazi ya Mkoa.

Maafisa waliojitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara ni Bibi Clevu Sepaku, Msimamizi wa Uchaguzi Kanda ya Ziwa Mashariki ambaye aliambatana na Bwana Mtibora Suleiman na Bwana Frank Shija.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.