• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Malima awataka wananchi kuwasilisha malalamiko

Posted on: February 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka wananchi na wadau mbalimbali wa mahakama kuwasilisha malalamiko yanayohusu maadili ya maafisa wa mahakama kwenye kamati ya Mkoa ya kushughulikia malalamiko hayo ili yaweze kufanyiwa kazi kwa mujibu ya sheria.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Februari 2021 wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na masuala mbalimbali ya maendeleo kwa Mkoa wa Mara.

“Natoa wito kwa wananchi wote wenye malalamiko yanayohusu maadili ya maafisa wa mahakama kuwasilisha malalamiko yao kwa maandishi na kamati yangu itatenda haki ya kusikiliza pande zote mbili zinazohusika kabla ya kutoa mapendekezo kwa Jaji Mfawidhi” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 50 cha Sheria ya Utumishi wa Mahakama Namba 4 ya mwaka 2011 kamati ya maadili inaongozwa na yeye kama mwenyekiti wake na wajumbe wengine sita ambao ni pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa ambaye ndiye kaatibu wa kamati hiyo.

Ameeleza kuwa majukumu ya kamati ya maadili wa maafisa wa mahakama ni kuchunguza malalamiko ya ukiukwaji wa maadili dhidi ya mahakimu na wasaidizi wa sheria wa majaji na kufanya maamuzi na kuandaa repoti ya uchunguzi wa malalamiko.   

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima wananchi wanaweza kulalamikia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na namna kesi ilivyoshughulikiwa; tuhuma za rushwa; kushindwa kutekeleza majukumu na vitendo vinavyokiuka kanuni za maadili ya maafisa wa mahakama.

Aidha amewataka wananchi kutoa malalamiko yao kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ndani ya miezi sita baada ya tukio kutokea kwa maandishi na kwa lugha ya Kiswahili ili kamati iweze kuyafanyia kazi malalamiko yao.

Mheshimiwa Malima ameahidi kamati hiyo kutenda haki katika kusikiliza na kushughulikia malalamiko yatakayowasilishwa kabla ya kutoa mapendekezo ya kamati kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.