• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Makungu awataka viongozi kushiriki maandalizi ya Dira 2050

Posted on: July 21st, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu amewataka viongozi wa Mkoa wa Mara kushiriki kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi na wadau wengine kushiriki kutoa maoni katika uandaaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025/2050.

Akizungumza katika ufunguzi wa warsha ya kuhamasisha ushiriki wa wadau katika maandalizi ya Dira hiyo, Bwana Makungu ameeleza kuwa warsha hiyo imelenga kutoa elimu kwa viongozi na wawakilishi wa makundi ya wadau kuhusu dira hiyo na utekelezaji wake pamoja na mchakato wa maandalizi ya Dira ya 2050.

“Mnapaswa kushiriki kikamilifu katika warsha hii kwa lengo la kuwa na uelewa wa pamoja na kuelewa majukumu yenu ya msingi ili kufanikisha shughuli hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa letu” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amesema kuwa wajumbe wa timu ya uandishi watasambaza nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, vipeperushi, mabango kuhusu maandalizi ya Dira 2050 na kutembelea vyombo vya habari vilivyopo katika Mkoa wetu nah ii itasaidia kuongeza wigo wa watu watakaofikiwa pamoja na kuacha nyenzo zitakazosaidia kuendelea na uelimishaji wa umma.

Kwa upande wake, Bwana Servus Sagday, Kiongozi wa Timu ya Uandishi wa Dira 2050 kwa Kanda ya Ziwa amewataka viongozi kuelewa maana na umuhimu wa Dira na kusaidia katika utoaji wa elimu kwa wananchi wanaowaongoza katika maeneo yao.

“Ili kupata ushiriki wa wananchi wengi katika maandalizi ya Dira 2050 ni muhimu kwa viongozi kuwapa elimu kuhusu Dira 2050 na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa wananchi kushiriki ili kupata Dira itakayogusa maisha ya Watanzania wote” amesema Bwana Sagday.

Kwa upande wake Bwana Peter Soke, mjumbe wa timu ya Uandishi wa Dira 2050 ameesa kuwa katika kupata maoni ya wadau njia mbalimbali zitatumika ikiwa ni pamoja na madodoso, mahojiano ya vikundi, vikao vya majadiliano na mahojiano maalum na baadhi ya watu.  

“Ili kupata maoni ya wadau wengi zaidi tutatumia pia mitandao ya simu na online portal ili kuwawezesha wananchi wengi kutoka maeneo mbalimbali kushiriki na kutoa maoni kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050” amesema Bwana Soke.

Bwana Soke ameeleza kuwa Dira ya Maendeleo ya Taifa inayotumika sasa ilianza mwaka 2000 hadi 2025 ikiwa na lengo kubwa la kuiwezesha Tanzania kuingia Uchumi wa Kati na Maisha bora kwa Kila Mtanzania na kuongeza kuwa kwa kiasi kikubwa Dira hii ilifanikiwa.

Ameeleza kuwa lengo la kuandaa Dira mpya ni kuendeleza malengo ya awali, kupata mwelekeo na mpango wa Taifa na ili kuendana na mabadiliko mbalimbali yaliyopo na yanayotarajiwa katika jamii kwa kipindi hicho.

Bwana Soke amewataka viongozi walioshiriki katika mkutano huo kushiriki katika kutoa elimu kwa wananchi na zoezi la ukusanyaji wa maoni ya wananchi katika maeneo yao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Mara Bwana Iddi Hamisi Mtani ameeleza kuwa ili kupata maoni ya watu wenye ulemavu, mbinu mbalimbali zinatakiwa kutumika ili kuwawezesha watu wenye ulemavu kuweza kutoa maoni.

Bwana Mtani amesema watahitajika wakalimani kuwasaidia watu wenye ulemavu wa kusikia, maandishi ya nukta nundu na maandishi manene kwa walemavu wenye matatizo ya kuona, kuangalia mazingira rafiki ya kuhojiwa kwa walemavu wa viungo na ngozi.

“Inafaa kuangalia mahitaji halisi ya watu wenye ulemavu na kuyajumuisha katika mipango ya jumla ya maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Taifa 2050 kutokana na changamoto mbalimbali za watu wenye za walemavu” amesema Bwana Mtani.

Warsha ya kutoa elimu kwa viongozi ilihudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Sehemu na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na baadhi ya wakuu wa idara za Halmashauri.

 Wengine waliohudhuria warsha hiyo ni viongozi wa dini, vyama vya siasa, viongozi wa vyama vya watu wenye ulemavu na mashirika yasiyo ya kiserikali na waandishi wa habari.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.