• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Makungu ataka mabadiliko sekta ya afya

Posted on: January 27th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amefanya kikao na wasimamizi wa afya katika Halmashauri na Wakuu wa Vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara na kuwataka kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya.

Akizungumza katika kikao hicho Bwana Makungu ameeleza matamanio yake kuwa Mkoa wa Mara uwe Mkoa wa mfano katika utoaji wa huduma bora za afya na mikoa mingine waje kuiga Mara.  

“Sisi tuwe Mkoa ambao unatoa huduma bora za afya, huduma nzuri na kwa wakati, lugha nzuri kwa wagonjwa, tufanye kazi kama timu moja ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazotukabili na kujenga uhusiano mzuri katika maeneo yetu ya kazi, tutafanikiwa” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amewataka wasimamizi na wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao ili kuwa wa mfano kwa watumishi waliochini yao na kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya havigeuki kuwa vituo vya malalamiko ya wananchi.

Aidha, Bwana Makungu amewahimiza watumishi woe wa sekta ya afya kuisaidia Serikali katika kutekeleza sheria ya mtoto ambayo inapiga marufuku vitendo vya ukeketaji katika jamii ili kuwanusuru watoto wakike kutokana na ukeketaji.

Bwana Makungu amewahimiza watumishi kuzijua sheria za utumishi wa umma ili kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Katibu Tawala amewahimiza wasimamizi wa sekta ya afya na wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya kutoa elimu kwa wananchi wote kuhusiana na umuhimu wa Bima ya Afya ili wananchi waweze kujiunga na kupata huduma za afya kwa urahisi zaidi.

Wakati huo huo, Bwana Makungu amewataka wasimamizi wa sekta ya afya kuhakikisha mifumo ya kukusanya mapato katika vituo vya kutolea huduma za afya inafungwa sehemu zote muhimu na inafanyakazi ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Zabron Masatu amemshukuru Katibu Tawala kwa kutenga muda wake kuzungumza na wasimamizi wa sekta ya afya na kuahidi kuyafuatilia mambo yote yaliyozungumzwa katika kikao hicho.

Akizungumza kuhusiana na rasimu ya Mfuko ya Bima ya Afya kwa wote, Dkt. Masatu amesema mfuko huu utakuwa ni mkombozi wa watanzania walio wengi katika kupata huduma za afya za uhakika wakati wote wanapohitaji.

Dkt. Masatu amewataka wasimamizi wa afya katika Halmashauri kutoa elimu kuhusu mpango wa serikali kwa wananchi ili waweze kuelewa na kuchukua hatua za kuunga mkono juhudi za serikali kuboresha huduma za afya.

Katika kikao hicho pia watumishi walipata nafasi ya kusikilisha wasilisho la Shiria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na rushwa katika mazingira ya kazi.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.