• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Makungu ahimiza wafanyakazi kutoa ushirikiano

Posted on: August 5th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo tarehe 5 Agosti, 2022 amewasili na kukabidhiwa ofisi na baadaye kuzungumza na Wakuu wa Vitengo na Idara pamoja na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara katika Ukumbi wa Uwekezaji.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na Wakuu wa Vitengo na Idara na wafanyakazi wakati wa makabidhiano hayo, Bwana Msalika amewahimiza wafanyakazi kutoa ushirikiano baina yao na kati yao na viongozi katika utekelezaji wa majukumu.

“Ninaomba tuendelee na ushirikiano uliopo na ili tutekeleze majukumu yaliyo mbele yetu kwa ufanisi katika kuzisimamia Halmashauri za Mkoa wa Mara” alisema Bwana Msalika.

Bwana Msalika ameeleza kuwa kwa sasa kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ni kuongeza makusanyo ya ndani ya Halmashauri na kuwataka wafanyakazi kusimamia kwa weledi makusanyo ya Halmashauri.

Aidha, Bwana Msalika amewataka wafanyakazi kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Kwa upande wake, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela amewashukuru wafanyakazi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano wao katika kutekeleza majukumu.

“Ninawashukuru sana kwa ushirikiano mlionionyesha wakati wote nilipokuwa hapa, ninawaomba muendelee na ushirikiano huo kwa Katibu Tawala mpya ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa urahisi zaidi” alisema Bwana Msovela

Katika tukio hilo, Bwana Msovela alimkabidhi ofisi Bwana Msalika tukio ambalo lilitanguliwa na kikao cha Katibu Tawala na Wakuu wa Idara na Vitengo na baadaye kikao na wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Aidha, katika tukio hilo wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa ametoa zawadi kwa Bwana Msovela na wamemkaribisha Bwana Msalika ambaye amewasili leo.

Bwana Msalika aliteuliwa na Rais tarehe 28 Julai, 2022 kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ambaye anachukua nafasi ya Bwana Albert Gabriel Msovela ambaye amehamishiwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma.  

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.