• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MARA REGION

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MARA REGION

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organisation Structrure
    • Sections
      • Planning & Coordination
      • Education Sector
      • Water Services
      • Economic & Productive
      • Admin AND Human Resource Management
      • Health & Social Welfare
      • LGAs Management Services
      • Infastructure
    • Units
      • Legal Services
      • Finance & Accounts
      • Internal Audit
      • Information & Communication Technology
      • Procurement & Supply Management
  • District
    • Musoma District
    • Butiama District
    • Bunda District
    • Rorya District
    • Tarime District
    • Serengeti District
  • Council
    • Musoma Muncipal
    • Bunda DC
    • Bunda Town
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Town
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Investment Opportunities
  • Services
    • Water
    • Education
    • Health
    • Infastructure
    • ICT
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Policies
    • Application Forms
    • Integrity Pledge Form
    • Client Service Charter
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Makungu agawa magari Sekta ya Afya

Posted on: December 19th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amegawa magari matatu kwa Hospitali ya Rufaa Kubukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) na Chuo cha Maafisa Tabibu Musoma yaliyotolewa na serikali yenye lengo la kuboresha usimamizi wa Sekta ya Afya.

Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo, Bwana Makungu amewataka wahusika kutumia magari hayo kwa mujibu wa maelekezo ya matumizi yake yaliyokusudiwa na Serikali.

“Ni mategemeo ya Serikali kuwa magari haya yatatumika kama ilivyokusudiwa na yataimarisha utoaji wa huduma katika Sekta ya Afya” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amesema gari moja la kisasa la kubebea wagonjwa na gari moja la usimamizi yametolewa kwa ajili ya Hospitali ya Kwangwa wakati gari moja ya usimamizi imetolewa kwa ajili ya Chuo cha Maafisa Tabibu Musoma.

Bwana Makungu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan,  Wizara ya Afya na Serikali kwa ujumla kwa kuuwezesha Mkoa wa Mara kwa vitendea kazi .

Aidha, Bwana Makungu ameeleza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya tayari imeshanunua magari mengine mawili kwa ajili ya Hospitali ya Kwangwa ambayo yatafika muda wowote kuanzia sasa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Maafisa Tabibu Musoma Dkt. Agustine Johnson ameishukuru Serikali kwa kukipatika Chuo hicho gari jipya ambalo amesema litaongeza nguvu katika ufundishaji wa mafunzo kwa vitendo.

“Kwa sasa Chuo kina gari moja tu na tuna wanachuo 400 ambao mara kwa mara wanahitaji kufanya mafunzo kwa vitendo katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya pamoja na kufuatilia mitihani ya wanachuo gari hili lilikuwa halitoshi” amesema Dkt. Johnson.

Dkt. Johnson ameiomba Serikali kukinunulia Chuo hiki basi dogo ili kurahisisha ufanyaji wa mafunzo kwa vitendo kwa wanachuo.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere amesema kuwa hospitali ilikuwa inachangamoto ya gari la kubebea wagonjwa lenye uwezo wa kwenda umbali mrefu kama vile Dodoma au Dar es Salaam na sasa gari hii wanategemea kuitumia kwa ajili hiyo.

Aidha, amesema gari hiyo ya wagonjwa ni ya kisasa na imewekewa vifaa tiba, mifumo ya gesi na inauwezo wa kufanya upasuaji mdogo kwa mgonjwa gari ikiwa njiani na hivyo kuokoa maisha ya wagonjwa wakiwa wanasafirishwa kwenda kwenye matibabu ya rufaa.

Aidha, amesema gari ya usimamizi itatumika kutembelea vituo vya kutolea huduma vilivyopo ili kutoa utaalamu na  ushauri kwa watoa huduma waweze kuboresha utoaji wa huduma za afya.

 Magari yaliyotolewa ni sehemu ya magari 31 ambayo Mkuu wa Mkoa wa Mara aliyatolea taarifa tarehe 23 Novemba, 2023 kuhusiana na mgao wa magari na vifaa tiba na baadhi ya magari hayo bado hayajapokelewa.

Announcements

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • View All

Latest News

  • Kongamano la Maonesho ya Madini kufunguliwa Mara leo

    June 03, 2025
  • Mtambi ataka ubunifu vyanzo vya mapato

    June 03, 2025
  • Mtambi aipongeza Musoma DC kupata hati safi

    June 03, 2025
  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • View All

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
More Videos

Quick Links

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Related Links

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Postal Address: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Telephone: +255282622305

    Mobile:

    Email: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2017 Mara Region . All rights reserved.